Wachezaji wa
Chelsea wakimrusha juu koch wao, Antonio Conte kwa furaha baada ya
kujihakikishia Ubingwa wa Ligi Kuu ya England Msimu huu wa 2016/2017 kufuatia ushindi wa 4-3 dhidi ya
Watford usiku wa Jumatatu May 15,2017 Uwanja wa Stamford Bridge.
Mabao ya
Chelsea yalifungwa na John Terry dakika ya 22, Cesar Azpilicueta dakika ya 36,
Michy Batshuayi dakika ya 49 na Cesc Fabregas dakika ya 88 wakati ya Watford
yamefungwa na Etienne Capoue dakika ya 24, Daryl Janmaat dakika ya 51 na
Stefano Okaka dakika ya 74.
Chelsea
imefikisha pointi 90 baada ya kucheza mechi 37 na sasa rasmi ni mabingwa wapya,
wakirithi taji lililoachwa wazi na Leicester City waliolibeba msimu wa 2015/2016.
|
John Terry
aweka rekodi.
Pamoja na
beki huyo kutokuwa na nafasi katika klabu ya Chelsea msimu huu lakini amekuwa
kapteni wa kwanza katika historia ya ligi kuu Uingereza kubeba makombe mengi
akiwa na matano, anayemfuatia ni Roy Keane mwenye manne.
|
Ubingwa huo
wa Chelsea umeifanya klabu hiyo kuwa na makombe 5 sawa na Manchester United na
kuzifanya timu hizo kuongoza kwa idadi ya makombe ya EPL tangu msimu wa mwaka
2003/2004.
|
No comments:
Post a Comment