Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, IGP Simon Sirro kwa mara ya kwanza
amefanya mazungumzo maalum na wanahabari Leo May 31,2017 jijini Dar es Salaam
ikiwa ni siku mbili tangu Amri Jeshi Mkuu wa nchi, Rais Dkt. John Pombe
Magufuli amuapishe kuwa IGP.
Katika mazungumzo yake, IGP Sirro amesema suala la mauaji kwa viongozi wa
Serikali za Mitaa yanayofanywa na wahalifu wilayani Rufiji, Kibiti, Ikwiriri na
Mkuranga Mkoa wa Pwani ni jambo la muda mfupi ambalo hivi karibuni majibu
sahihi yatapatikana.
“Wanahabari niseme tu kwamba nchi yetu ni shwari,
hatuna matukio makubwa ya kutisha, lakini changamoto kubwa ni Mkoa wa Pwani
ambako baadhi ya raia wema wameuawa bila sababu, kuna kikundi cha watu wachache
wanaodhani wanaweza kuufanya ule mkoa kukosa amani. Lakini haki lazima itatoa
majibu.
“Niwahakikishie Watanzaia kwamba suala la Ikwiriri,
Mkuranga na Rufiji ni la muda mfupi, viongozi wangu wamezungumza ukianza na
Rais (Dkt. John Pombe Magufuli), Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi (Mwigulu
Nchemba) hivyo mimi sina la kuzungumza zaidi ya kufanya kazi kwa weredi.
“Aidha Sirro amesema Jeshi la Polisi linapeleka
salam kuwa ubaya wanaoufanya na wahalifu huko Pwani, wataujibu kwa ubaya kwa
mujibu wa sheria. Amesema IGP SIrro.
Kuhusu wanaotumia bodaboda kufanya uhalifu, amesema hakuna mtu alie juu
ya sheria. Amesema bodaboda wanapita kwenye taa nyekundu, wanapita wakiwa
kwenye mshikaki. Amewapa salam kuwa ni wakati wa utii wa sheria.
Sirro amewaonya watu wanaojihusisha na madawa ya kulevya.
Watu wenye hasira kali nao wameguswa akitolea mfano wezi wa kuku na
kuhoji kama kuku ana thamani sawa na mhusika. Amesisitiza kama amekosa akamatwe
na apelekwe mahakamani na kusema anayejifanya ana hasira kali itamfanya aiache
familia yake.
Kuhusu askari kujihusisha na rushwa, amesema hakuna askari
atakaejihusisha na Rushwa na akabaki salama na kusema ameshatoa maelekezo kwa
jeshi polisi kuwa atakaefanikisha kupatikana kwa wala rushwa atapata zawadi.
Sirro pia ameahidi kutoa shilingi milioni 10 kwa raia mwema atakayetoa
taarifa sahihi kwa watu wanaotekeleza mauaji Kibiti, Mkuranga, Rufiji na
Ikwiriri Pwani.
BONYEZA
PLAY HAPA CHINI KUMSIKILIZA IGP Sirro AKIZUNGUMZA
No comments:
Post a Comment