Wanafunzi wa
shule ya sekondari ya Mtakatifu Alfed Rulenge hujishughulisha na elimu ya
ujasiliamali ambapo hutengeneza sabuni za maji na miche wakiongozwa na mwalimu
wao wa ujasiliamali Godbert Kalezibwaki , kwa ajili ya usafi wa mavazi na
kusafisha miundombinu mbalimbali kama vyoo, ambapo kwa sasa wanahitaji usajili
baada ya kukaguliwa na TBS
Picha/
HABARI na Shaaban Ndyamukama.
|
Katika hatua
nyingine Mgeni rasmi kwenye mahafali hayo Meneja wa benki ya CRDB Tawi la Ngara
mkoani Kagera Ernest Chacha amewahimiza wahitimu kufanya kazi halali zenye kuwaongezea mapato kiuchumi
ambapo amefurahia uanzishwaji wa elimu ya ujasiliamali shuleni hapo.
Akihutubia
wanafunzi na wahitimu pamoja na wazazi au walezi waliohudhuria mahafali hayo
Meneja huyo ameendesha harambee ya
kupunguza changamoto za miundombinu na
kupatikana kiasi cha Sh1.2 milioni naye kuchangia kiasi kama hicho akiahidi
kuingiza fedha hizo kwenye akauti ya shule itakayofunguliwa kupitia benki ya
CRDB.
|
Jumla
ya wanafunzi 25 wa kidato cha sita
wamehitimu kidato hicho shuleni hapo kati yao ni wasichana tisa na wavulana 16
baada ya kuanza mwaka 2015 wkiwa
wanafunzi 32 kati yao wavulana 21 na wasichana 11 lakini baadhi yao hawakuweza
kuhitimu kutokana na sababu mbalimbali za kimazingira.
|
No comments:
Post a Comment