Shule mpya
ya msingi Rubondo iliyoko Kitongoji cha Nyarukongogo Mamlaka ya mji mdogo wa Biharamulo
Mkoani Kagera.
|
Mwenyekiti
wa Halmashauri ya wilaya ya Biharamulo,Mhe.
Afsa Galiatano na Mkurugenzi wa halmashauri hiyo Bi.Wende Ng'ahala wakikagua
ujenzi wa madarasa manane na matundu 20
ya vyoo ya shule mpya ya msingi Rubondo
iliyoko Kitongoji cha Nyarukongogo Mamlaka ya mji mdogo wa Biharamulo Mkoani
Kagera.
Walikagua
madarasa hayo manane na vyoo vya wanafunzi 900 watakaohamia katika madarasa
hayo mapya baada ya kuboresha ya awali ambayo walisoma kwa msongamano wa
wanafunzi 80 darasa moja na sasa watakuwa ni wanafunzi 45 ambapo ujenzi
umegharimu Sh 190 Milioni.
|
Pia shule
hiyo imewekewa miundombinu ya maji na umeme na madawati 240 yenye thamani ya
Sh12mil na imejengwa kwa kutumia wakandarasi, mafundi na vibarua wa
kawaida wakiwa ni wazaliwa wa kitongoji
hicho ambacho awali kilikuwa ni kijiji kabla ya kuwa ndani ya Mamlaka ya Mji wa
Biharamulo
|
Mwenyekiti
huyo wa Halmashauri na Mkurugenzi walikagua ujenzi wa madarasa hayo jana na
kushauri Mwenyekiti wa kamati ya shule Mathias kagimba kuharakisha ukamilishaji
wa miundombinu ili wanafunzi wahamie kwenye madarasa hayo ifikapo Julai mwaka
huu.
Habari/Picha Na-Shaban Nasib Ndyamukama.
|
No comments:
Post a Comment