Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia majina hayo
pamoja na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan
mara baada ya kufungua boksi kubwa lenye majina ya watumishi hao wa umma
ambao wamegushi vyeti vyao .
|
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akikata utepe katika
vitabu hivyo vya taarifa ya zoezi la uhakiki wa vyeti kwa watumishi wa umma alivyopokea kutoka kwa
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala bora
Angela Kairuki katika Ukumbi wa Chimwaga mjini Dodoma. Katikati ni Makamu wa
Rais Samia Suluhu Hassan na wakwanza kushoto ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha
Dodoma (UDOM) Profesa Idris Kikula.
|
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan,
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa , Waziri wa Elimu Profesa Joyce Ndalichako, Spika
wa Bunge Job Ndugai, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa
Umma na Utawala bora Angela Kairuki wakiminya kitufe kuashiria maadhimisho ya
miaka 10 ya Chuo Kikuu cha Dodoma UDOM katika ukumbi wa Chimwaga mkoani Dodoma.
|
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia viongozi mbalimbali, wanafunzi wa
UDOM, pamoja na watumishi wa Umma mara baada ya kupokea Taarifa ya zoezi la
uhakiki wa vyeti kwa watumishi wa umma
kutoka kwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na
Utawala bora Angela Kairuki katika Ukumbi wa Chimwaga mjini Dodoma.
|
Baadhi ya
Makatibu wakuu pamoja na viongozi mbalimbali wa Serikali wakifatilia kwa makini
hotuba iliyokuwa ikitolewa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John
Pombe Magufuli katika ukumbi wa Chimwaga mkoani Dodoma.
|
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akagana na watumishi
mbalimbali wa umma, viongozi pamoja wanafunzi wa UDOM mara baada ya kumaliza
kuhutubia katika Ukumbi wa Chimwaga mjini Dodoma.
|
No comments:
Post a Comment