Serikali
imesema jumla ya walimu 3,081 wakiwemo walimu 7 wa shule ya Sekondari Omumwani
Kagera, wameajiriwa, hivyo bado kuna nafasi ya walimu 1.048 kati ya nafasi
4,129 za walimu wa Sayansi na Hisabati zilizotolewa kibali cha ajira.
Taarifa hiyo
imetolewa leo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za
Mitaa (TAMISEMI) George Simbachawene alipokuwa akizungumza na
Waandishi Habari,ofsini kwake ambapo amewataka walimu wote walioajiriwa
wanatakiwa kuripoti katika vituo vyao vya kazi kuanzia tarehe 18 hadi 25 mwezi
huu.
Amesema walimu
walioajiriwa wamepangwa moja kwa moja na TAMISEMI katika halmashauri zote
nchini ambazo zina upugufu wa walimu wa Sayansi na Hisabati.
Simbachawene
amesema kati ya walimu hao walioajairiwa walimu 1,537 ni wa Shahada na
walimu 1,544 ni wa Stashahada.
“Sehemu
kubwa ya walimu wa Shahada wamepangwa kwenye shule za kidato cha tano na
sita na wachache kwenye shule za kidato cha kwanza hadi cha nne’’ alisema.
Simbachawene
amekiri kuwa kuna upungufu wa walimu 26,026 wa masomo Sayansi na Hisabati
katika shule mbalimbali za sekondari nchini.
“Moja ya
changamoto kubwa ambazo zinaikabili sekta ndogo ya elimu ya sekondari ni
upungufu wa walimu wa Sayansi na Hisabati upungufu uliopo katika shule
3,602 ni 26,026 sawa na asilimia 60.14 ya walimu 43,248 wanaohitajika” amesema
Simbachawene
Amesema
walimu wanaohitajika kwa masomo hayo ni walimu 43,248 lakini waliopo kwa sasa
ni 17,252 pekee.
Amesema kwa
sasa serikali ina shule za sekondari 3,602 na kati ya hizo shule 333 ni za
kidato cha tano na sita huku zingine 54 za kidato cha tano zimeanzishwa .
Aidha
amesema shule hizo za sekondari kwa upande wa masomo ya Sanaa ina ziada ya
walimu 7,463 ambapo waliopo ni walimu 63,240 na wanaohitajika ni walimu 55,777.
“Kutokana na
ziada hiyo ya walimu wa Sanaa serikali imeanza kuchukua hatua yawahamisha
walimu hao katika shule za msingi ili kuziba upungufu wa walimu katika shule
hizo’’ alisema.
|
No comments:
Post a Comment