Ligi Kuu ya
Vodacom Tanzania Bara (VPL) inatarajiwa kuendelea kuanzia Kesho Alhamisi April
13, 2017 kwa timu ya Mbeya City itaikaribisha African Lyon ya Dar es Salaam
kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya katika mchezo utakaoanza saa 10.00 jioni.
Jumamosi ya
Aprili 15, mwaka huu,2017 kutakuwa na michezo minne ambako Stand United itakuwa
mwenyeji wa Mtibwa Sugar ya Morogoro kwenye Uwanja wa Kambarage mkoani
Shinyanga wakati Toto Africans ya Mwanza itaialika Simba SC ya Dar es Salaam
kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza. Mechi hizi, zitachezwa kuanzia saa
10.00 jioni.
Kadhalika
siku hiyo ya Jumamosi, Majimaji FC ya Songea itakuwa mgeni wa Ruvu Shooting ya
Pwani kwenye Uwanja wa Mabatini mkoani Pwani - mchezo utakaoanza saa 8.00
mchana ilihali JKT Ruvu ikiwa kwenye Uwanja wake mpya wa nyumbani - Mkwakwani
jijini Tanga itaialika Azam FC ya Dar es Salaam kuanzia saa 10.00 jioni.
Kwa mujibu
wa ratiba, Jumapili Aprili 6, mwaka huu,2017 Mbao FC itacheza na Tanzania Prisons
kwenye Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza huku Mwadui FC ikiwa mwenyeji wa Ndanda
FC ya Mtwara kwenye Uwanja wa Mwadui mkoani Shinyanga. Kadhalika, mechi hizo
zitaanza saa 10.00 jioni.
IMETOLEWA NA
TFF
|
No comments:
Post a Comment