Mke wa Rais
Mama Janeth Magufuli akichota mchanga na kuweka kama ishara ya kushiriki katika
ujenzi huo wa Reli ya Kisasa Standard Gauge itakayoanzia jijini Dar es Salaam
hadi mkoani Morogoro na baadaye kuendelea hadi Kigoma na Mwanza
|
Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiangalia majina ya
baadhi ya wataalamu mbalimbali waliohusika katika mchakato wa Ujenzi huo wa
Reli ya Kisasa Standard Gauge itakayoanzia jijini Dar es Salaam hadi mkoani
Morogoro na baadaye kuendelea hadi Kigoma na Mwanza. Wakwanza kulia ni Kaimu
Mkurugenzi Mtendaji wa kampuni hodhi ya Rasilimali za Reli (RAHCO) Masanja
Kadogosa akiwa ameshika majina hayo.
|
Rais wa
Tanzania,Dkt John Pombe Magufuli amezindua Rasmi ujenzi wa Mradi wa Reli ya
Kisasa ya Kimataifa ambayo treni ya kisasa inayotumia umeme itaweza kusafiri
kwa mwendokasi wa kilomita 160 kwa saa.
Akizungumza
wakati wa uzinduzi wa mradi huo, Mkurugenzi wa RAHCO alianza kwa kueleza;
“Reli ya
kisasa itakayojengwa, treni itaweza kusafiri kwa KM 160/saa, na itatumia umeme
na mafuta. Treni itaweza kutoka Dar kwenda Dodoma kwa saa 2 na dakika 50, Dar –
Mwanza kwa saa 7 na dakika 40.
“Treni
itakuwa na urefu wa Km 2, sawa na semitrailer 500 na itakuwa na mabehewa 100.
Iwapo dereva atakiuka taratibu, muongozaji aliyeko Dar anaweza kuizima treni
hata kama ipo Mwanza.
|
“Kutajengwa
mifumo ya mawasiliano na ya mizigo njiani, itaweza kubeba tani milioni 15 kwa
mwaka. Ujenzi wa Reli hiyo utafanyika kwa muda wa miezi 30 hadi kukamilika.
“Ujenzi wa
Reli hiyo utagharimu dola bilioni 1.29 bila kodi na dola bilioni 1.8 pamoja na
kodi. Sehemu za milima patajengwa madaraja ili treni iweze kupita kirahisi.
Treni itaweza kutoka Dar kwenda Dodoma kwa saa 2 na dakika 50, Dar – Mwanza kwa
saa 7 na dakika 40.
|
Rais
Magufuli amemtaka mkandarasi wa mradi huo kuhakikisha kuwa ikiwezekana
anaumaliza mradi kabla ya miezi 30 ili wananchi waondokane na adha ya usafiri.
Aidha Rais
ameongeza kuwa ni Tanzania pekee kwa nchi zote za Afrika ambayo imeweza kujenga
mradi wa reli kama huo kwa pesa zake za ndani.
Rais
Magufuli pia ameagiza ujenzi wa Reli hiyo ya kisasa ya Dar-Morogoro
utakapoanza, ajira zote wapewe wakazi wa Pugu.
|
No comments:
Post a Comment