Picha/Habari Na:Sylvester M. Raphael-Kagera.
|
Pia Bw.
Martine Loibook Kaimu Mkurugenzi wa
Mamlaka ya Wanyamapori Tanzania alikabidhi ndege mbili zisizotumia rubani
(Drones) zenye thamani ya dola 40,000 USD
(Dola elfu arobaini) na kusema kuwa TAWA wamefurahishwa na jinsi
Serikali ya Mkoa wa Kagera ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa Mhe. Kijuu inavyoendelea
na zoezi la operesheni ili kunusuru Hifadhi za Misitu na Wanyamapori.
Meja
Jenerali Mstaafu Hamis Semfuko naye pia alisema lengo la kutoa vifaa hivyo ni
kuhakikisha operesheni inafanikiwa kwa asilimia mia moja na vifaa hivyo vitasaidia kufanya operesheni
kila eneo la Hifadhi la Mkoa wa Kagera bila kuacha wavamizi na mifugo katika
maeneo hayo.
|
Kwaniaba ya
Serikali Mkoani Kagera Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Kagera Mhe. Deodatus Kinawilo
ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Bukoba alivipokea vifaa hivyo na alishukuru
kwaniaba ya Serikali ya mkoa kuwa vifaa vilivyotolewa kuwa vitaongeza ufanisi
katika operesheni hiyo.
Aidha Kaimu Mkuu wa Mkoa aliendelea kutoa rai kuwa
operesheni hiyo siyo nguvu ya soda bali maeneo yote ya hifadhi za Misitu na
Wanyamapori yatasafishwa ili yabakie kama ilivyokuwa awali.
Aidha Bw.
Faustine Masalu Mkurugenzi wa Huduma za Ulinzi na Usimamizi wa Wanyamapori
Tanzania ambaye ni Mtekelezaji Mkuu wa Operesheni alisema operesheni inaendelea
vizuri ambapo tayari watuhumiwa 19 na jumla ya mifugo 1922 ilikuwa imekamatwa
kufikia April 2, 2017 Jumapili jioni.
|
No comments:
Post a Comment