Waziri mkuu
Mh. Kassim Majaliwa pamoja na wabunge mbalimbali wameshiriki kuuaga mwili wa
aliyekua mbunge wa Viti Maalum (CHADEMA) Dkt Elly Macha, aliyefariki nchini
Uingereza alipokuwa akipatiwa matibabu.
Mwili huo
umewasili alfajiri leo,April 21,2017 katika uwanja wa Mwalimu Nyerere ambapo
mapokezi yaliongozwa na Naibu spika wa Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa
Tanzania Dk Tulia Ackson na kusafirishwa tena mpaka Dodoma ambapo viongozi wa
bunge wamepata fursa ya kuuaga Mheshimiwa Macha kwenye viwanja hivyo vya bunge.
Dkt Macha
alifariki dunia Machi 31 mwaka huu katika hospitali ya New Cross, Wolverhampton
iliyopo nchini Uingereza alipokuwa akipatiwa matibabu.
Aidha Naibu
spika, Dk Tulia Ackson amesema Bunge lilipata taarifa za ugonjwa wa marehemu
ndani ya miezi mitatu na baadae kupata taarifa juu ya kifo chake na kusema
kwamba, licha ya kua na ulemavu, Dkt Macha alipigania haki za walemavu kijasiri
na kikamilifu.
|
No comments:
Post a Comment