Baada ya
kamati tendaji ya Yanga kupitia kwa mjumbe wake Salum Mkemi kutanganza kupinga
malalamiko ya Simba dhidi ya Kagera Sugar kwa kumtumia mchezaji wao Mohamed
Fakih kwenye mechi kati ya Kagera Sugar dhidi ya Simba, afisa habari wa Simba
Haji Manara ametoa taarifa rasmi akiwataka Yanga kutulia.
Kuna taarifa
iliyotolewa na klabu ya Yanga inayoonyesha kuishinikiza Bodi ya ligi
kutokutenda haki juu ya rufani yetu dhidi ya klabu ya Kagera Sugar kwa
kumchezesha mchezaji Mohammed Fakih aliyecheza dhidi yetu akiwa na kadi tatu za
njano ambalo ni kosa kisheria.
Taarifa hiyo
ya Yanga iliomnukuu Mjumbe wa kamati ya utendaji ya klabu hiyo Salum Mkemi
aliyeoongea mbele ya waandishi huku akiwa na katibu mkuu wa klabu hiyo Charles
Boniface Mkwasa iliitaka bodi kutokutoa points kwa Simba eti kwa kuwa hizo
points zitawaathiri Yanga kwenye kutetea ubingwa wao ambao kwa sasa upo rehani,
pia taarifa hiyo imeonyesha Yanga wanao ushahidi kuwa Fakih ana kadi mbili za
njano.
Klabu ya
Simba inawaambia viongozi wa Yanga wanayo mambo ya msingi ya kuwashughulisha,
ikiwepo kutafuta mishahara ya wachezaji wao iliokwama kwa miezi kadhaa kama
inavyoripotiwa mitandaoni na kwenye vyombo vya habari,pia waangalie namna bora
ya kuurejeshea hadhi uwanja wake wa mazoezi wa Kaunda ili upate kuchezeka tena
na sio ulivyo hivi sasa,ambapo umegeuka kama bwawa la kufugia kambale,,ni
kushangazwa kulikochupa mpaka kufuatilia rufani isiyowahusu,Hii ni rufani ya
Simba dhidi ya Kagera sio wao Yanga.
Tunaamini
bodi haitafanya maamuzi kwa shinikizo la yoyote yule,na hatutarajii kuona
porojo walizozisema leo zitaondoa ukweli uliopo mezani kwao ambao klabu yetu
imeuwasilisha
Mwisho
niwaombe washabiki wetu watulie na waiachie bodi ifanye maamuzi yake ambayo
tunaamini yatatoa haki kwa anayestahili.
IMETOLEWA
NA.. Haji S Manara
Mkuu wa
Habari wa Simba Sc
SIMBA NGUVU
MOJA
|
No comments:
Post a Comment