Hatua Zilizochukuliwa.
Watuhumiwa
19 tayari wamekamatwa na kufikishwa Makamani kwa makosa mbalimbali ya kuendesha
shughuli za kibinadamu katika Misitu ya Hifadhi na Mapori ya Akiba ambapo
akitoa ufafanuzi mara baada ya kutoka Mahakamani Wakili wa Serikali Mwandamizi
Athumani Matuma Kirati akiambatana na Mawakili wenzake wawili wa Serikali
Erastus Anosisye na Haruna Shomari alisema;
“Ofisi ya
Mwanasheria Mkuu wa Serikali kufikia April 2, 2017 ilikuwa imepokea mafaili 12
yanayohusiana na makosa mbalimbali katika Hifadhi za Wanyamapori na Hifadhi za
Misitu ambapo watuhumiwa 19 wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya kwa makosa
ya kuingia bila kibali katika hifadhi, kuchunga mifugo katika hifadhi za Misitu
na Wanyamapori, kukutwa na mazao ya Misitu bila kibali na kukutwa na zana za
kuvunia mazao ya misitu kama misumeno na shoka.” Alifafanua Wakili Matuma.
Makosa mengine
ni kukutwa na vifaa vya kusafirishia mazao ya misitu kama baiskeli, na kuvuna mazao ya misitu (Kambapori) bila
kibali au idhini ya mamlaka husika. Katika kesi hizo 12 zilizofikishwa
mahakamani kesi tatu tofauti zilimalizika kwa watuhumiwa watano kukiri makosa
yao na kutozwa faini ya shilingi 100,000/= (laki moja) hadi shilingi 500,000/=
(laki tano) au kifungo cha mwaka mmoja kwa kila kosa.
|
Pia Wakili
Mwandamizi Matuma alisema ofisi ya Mwanansheria Mkuu wa Serikali inaendelea
kupokea mafaili mengine ya kesi na mara baada ya kuyapitia na kukaridhika na
vielelezo vya ushahidi watawasilisha
kesi hizo Mahakamani.
Kesi tatu zilizokamilika na kutolewa hukumu na Mahakama
ni Kesi namba 83, 85, 79 za mwaka 2017 ambapo jumla ya watuhumiwa watano
walikiri makosa yao na kuhukumiwa kamailivyotajwa hapo juu.
|
Kuhusu
mifugo iliyokamatwa Wakili Mwandamizi wa Serikali Bw. Matuma alisema kuwa
Mahakama itatoa uamuzi mara baada ya kutembelea maeneo ya mifugo ilikokamatiwa
na kuhifadhiwa katika hifadhi ili kujionea na kukubali kiwe kielelezo cha
ushahidi.
Kesi zote 12 ziliskilizwa na tatu kutolewa uamuzi na Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya
ya Biharamulo Niku Mwakatobe.
|
No comments:
Post a Comment