Mtu mmoja
katika kijiji cha Solwe wilayani Kwimba mkoani Mwanza anashikiliwa na jeshi la
polisi kwa tuhuma za kumuua mkewe kutokana na imani za kishirikina.
Tukio hilo
limetokea tarehe 5/04/2017 saa 5 asubuhi ambapo mtu huyo anayefahamika kwa jina
la Kumalija Kondolo Basu anadaiwa kumchoma mke wake na kitu chenye ncha kali
sehemu za kichwani na shingoni upande wa nyuma na kupelekea kifo chake papo
hapo.
Inadaiwa
kuwa mtuhumiwa alikuwa akiishi na mkewe nyumbani kwake kijiji cha Bagadu
wilayani Magu lakini hivi karibuni alikwenda kwa wakwe zake wilayani Kwimba
kuwasalimia yeye pamoja na mkewe.
Kamanda wa
Polisi Mkoa wa mwanza DCP Ahmed Msangi amesema kuwa siku ya tukio mtuhumiwa
alibaki nyumbani na mkewe kwani wengine walikuwa wamekwenda gulioni kwasababu ilikuwa siku ya gulio.
Kwa mujibu
wa Kamanda Msangi, inadaiwa kuwa baada ya mtuhumiwa kuona wanafamilia hawapo
ndipo alimchukua mkewe na kuingia naye ndani na kisha kutekeleza kitendo hicho.
Amesema
wananchi walitoa taarifa polisi kuhusiana na tukio hilo ambapo askari walifanya
ufuatiliaji wa haraka hadi eneo la tukio na kufanikiwa kumakamata mtuhumiwa.
Amesema
mtuhumiwa wa mauaji hayo amekamatwa na yupo katika mahojiano na jeshi la
polisi, pindi uchunguzi ukikamilika atafikishwa mahakamani.
|
No comments:
Post a Comment