Brazil
imerejea kileleni kwa mara ya kwanza baada ya Miaka 6 na hili limekuja baada ya
mafanikio makubwa chini ya Kocha wao Tite ambae ameshinda Mechi 9 mfululizo
tangu atwae wadhifa Mwaka Jana wakifunga Bao 25 na kufungwa 2 tu.
Hivi
karibuni Brazil ilishinda Mechi zake zote 2 za Kundi la Nchi za Marekani ya
Kusini na kuwa Nchi ya Kwanza kufuzu kuingia Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka
2018 huko Russia.
Wiki
iliyopita, Brazil kwanza iliifunga Uruguay 4-0 huko Montevideo na Siku 3 baadae
kuichapa 3-0 Paraguay huko Sao Paolo, Brazil.
Brazil
wameitoa Argentina kwenye Namba 1 ya Listi ya Ubora baada ya Argentina hivi
karibuni kushinda Mechi 1 tu, walipoifunga Chile 1-0, na kisha kuchapwa 2-0 na
Bolivia.
Argentina
sasa wameshika Namba 2 baada kukaa kileleni kwa Miezi 12 walipowang'oa Mabingwa
wa Dunia Germany ambao sasa wako Nafasi ya 3.
Katika 10
Bora Nchi pekee mpya ni Switzerland ambayo ipo wa 9 baada ya kuifunga Latvia
1-0 kwenye Mechi ya Kundi lao la Ulaya la kusaka kufuzu kucheza Fainali za
Kombe la Dunia za Mwaka 2018.
Nao Vigogo
Netherlands, baada ya Wiki hii kuchapwa na Bulgaria na Italy, wamezidi
kuporomoka kwa Nafasi 11 na kuangukia Nafasi ya 32 ikiwa ndio Nafasi ya chini
kabisa katika Historia yao.
Wengine
walioporomoka mno ni Uruguay walioshuka Nafasi 6 na kuangukia Nafasi ya 15
baada Wiki hii kuchapwa na Brazil na Peru.
Wakati Egypt
ndiyo Timu ya juu kabisa kwa Afrika ikishika Nafasi ya 19, Tanzania sasa ipo
Nafasi ya 135 ikitokea Nafasi ya 157 baada ya kuzifunga Botswana na Burundi
Nchi ambazo ziko juu yake.
FIFA LISTI
YA UBORA DUNIANI – 20 BORA.
1 Brazil
2 Argentina
3 Germany
4 Chile
5 Colombia
6 France
7 Belgium
8 Portugal
9 Switzerland
10 Spain
11 Poland
12 Italy
13 Wales
14 England
15 Uruguay
16 Mexico
17 Peru
18 Croatia
19 Egypt
20 Costa Rica
|
Thursday, April 06, 2017
FIFA Ubora wa Soka Duniani: Tanzania Yapanda Nafasi 22.
Tags
# MICHEZO
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
MICHEZO
Labels:
MICHEZO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment