1.Simon
Msuva.
Mcheza soka katika timu ya taifa Taifa Stars na pia winga wa klabu ya
Yanga SC, Simon Msuva anaongoza orodha hii, Msuva hadi sasa ana followers 207,000
na ndio mchezaji anayeongoza akiwa amewaacha wenzake kwa mbali sana.
2.Juma
Kaseja.
Golikipa wa Kagera Sugar ambaye pia amepitia vilabu vya Yanga SC na Simba
SC,Juma Kaseja yuko nafasi ya pili akiwa na idadi ya followers 115,000 katika
ukurasa wake wa Instagram.
3.Haruna
Nyionzima.
Wakati Msuva anaongoza kwa idadi ya followers instagram anayemfuatia
kwa idadi kubwa ya followers kutoka Yanga SC, ni Haruna Nyionzima, Mnyarwanda huyo
hadi sasa ana idadi ya followers 114,000 katika ukurasa wake wa Instagram.
4.Deus
Kaseke.
Yanga SC, tena wanakuja katika nafasi ya nne hii inamaanisha nne bora ni
mchezaji mmoja tu asiyetokea Yanga, Kaseke yupo katika nafasi hii akiwa na
followers 109,000 katika ukurasa wake wa Instagram.
5.Paul
Nonga.
Mshambuliaji wa Mwadui FC, anatokea katika nafasi ya tano, huyu ni Nonga
ambapo Nonga ana followers 101,000 katika ukurasa wake wa Instagram
6.Juma
Abdul.
Nafasi ya 6 pia ni Yanga SC, Juma Abdul yuko katika nafasi hii kwa kuwa na
followers 96,800 katika ukurasa wake huo wa Instagram.
7.Mohamed
Hussein.
Nafasi ya saba ndio kumetokea mchezaji wa kwanza ambaye ni Simba SC na ni
beki wa Simba SC Mohameid Hussein Tshabalala ambaye ana idadi ya followers 96,200
katika ukurasa wake wa Instagram.
8.Said
Ndemla.
Kiungo wa Simba SC, Saidi Hamisi Ndemla yuko katika nafasi ya 8 akiwa ana
followers 81,900 ikiwa ni pungufu ya followers 14,300 kutoka alipo Tshbalala.
9..Mrisho
Ngassa.
Nafasi ya tisa inashikiliwa na winga wa zamani wa klabu ya Yanga SC ambaye
kwa sasa anakipiga Mbeya City Mrisho Ngassa.
Ngassa anao followers 88,700
katika mtandao wake wa Instagram.
10.Himid
Mao.
Nafasi ya 10 ni kiungo mkabaji wa Azam FC, Himid Mao “Ninja”, Himid
ameingia katika kumi bora ya wasakata kabumbu wa Tanzania wenye followers wengi
akiwa na followers 74,400.
|
No comments:
Post a Comment