Zikiwa
zimebakisha mechi 6 za Ligi kuu soka Uingereza 2016/2017 kufikia tamati, kila mmoja Chelsea waliocheza mechi 32 ndio wapo kileleni wakiwa na Pointi 75
na kufuatia Tottenham Spurs wenye Pointi 71 kwa mechi pia 32.
Wikiendi hii
Chelsea na Spurs zitapambana kwenye Uwanja wa Wembley Jijini London kwenye
Mechi ya Nusu Fainali ya FA CUP Mechi ambayo inasemwa itatoa morali kwa Mshindi
kuelekea Ubingwa.
Kwa Mechi 6
zilizobaki kwa Timu hizi mbili, Tottenham Spurs ndio wanaonekana kuwa na Ratiba ngumu
kupita Chelsea kwani wanapaswa kuzivaa Arsenal, Man United na Mabingwa
Leicester City miongoni mwa Mechi zao wakati Chelsea, kimtazamo, Mechi yao
ngumu ni dhidi ya Everton tu.
EPL, Ligi
Kuu England 2016/2017– Mechi zilizobaki.
-U=Ugenini
N=Nyumbani
Tottenham Spurs –
Ratiba:
Aprili 22:
Chelsea [FA Cup Nusu Fainali, Wembley]
Aprili 26:
Crystal Palace [U]
Aprili 30:
Arsenal [N]
Mei 6: West
Ham United [U]
Mei 13 Man
United [N]
Mei 18
Leicester [U]
Mei 21: Hull
City [U]
Chelsea –
Ratiba:
Aprili 22:
Tottenham [FA Cup Nusu Fainali, Wembley]
Aprili 25:
Southampton [N]
Aprili 30:
Everton [U]
Mei 8:
Middlesbrough [N]
Mei 12: West
Brom [U]
Mei 15:
Watford [N]
Mei 21
Sunderland [N]
|
No comments:
Post a Comment