Na Daudi
Manongi-MAELEZO, DODOMA.
Serikali
kupitia Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji imeandaa Rasimu ya Muswada wa
Sheria itakayoweka bayana taratibu na mfumo wa usimamizi na udhibiti wa bishara
ya chuma chakavu katika hatua mbalimbali za uzalishaji, ukusanyaji, usambazaji,
uuzaji na uyeyushaji wake kwa kuzingatia uhifadhi na usimamizi wa mazingira kwa
manufaa ya Taifa.
Hayo
yalisemwa jana na Waziri wa
Viwanda,Biashara na Uwekezaji Mhe.Charles Mwijage wakati akijibu hoja
mbalimbali za wabunge Mjini Dodoma.
"Biashara ya Chuma chakavu imeshamiri hapa
nchini na duniani kwa ujumla na hili limetokana na mahitaji ya vyuma chakavu
ambapo kumetumiwa na wahalifu kuharibu miundombinu iliyojengwa kwa vyuma kwa
nia ya kupata chuma ili waiuze kama chuma chakavu" Alisema Mwijage.
Alisema ili
kukabiliana na hujuma hizi Mamlaka husika zikiwemo TANESCO, TANROADS na RAHCO
wamekuwa wakifanya kazi kwa karibu na jeshi la Polisi ikiwemo kutumia walinzi
wa Taasisi husika ili kulinda rasilimali hizo.
Alisisitiza
kuwa Muswada huu umeweka wazi na bayana adhabu itakayotolewa kwa mtu atakayebainika
kuharibu miundombinu.
Aidha
Mhe.Mwijage alitoa wito kwa watanzania kutoa taarifa pindi waonapo mtu
anayehujumu miundombinu kwa namna yote ile.
“Natoa wito kwa wenye viwanda na
wafanyabiashara wa vyuma chakavu
jiepusheni na ununuzi wa vyuma ambavyo asili yake ina mashaka na
tutaharakisha sheria hii ili kutatua tatizo hili,” aliongeza Mwijage.
|
No comments:
Post a Comment