Suala la mipaka ya kimataifa mara
zote huchukuliwa kama la kisiasa zaidi ya kitamaduni ambapo watu huwa
na utaratibu wa kuivuka kihalali au kwa njia za panya. Baadhi ya mipaka
inayozigawa nchi duniani huwa rahisi baina ya mataifa, wakati mwingine
huwa na uzio, patrols, na vitisho vya vifo au kifungo kwa wasioiheshimu.
Worldatlas imetoa list ya nchi 10
zilizopakana na nchi nyingi zaidi huku China ikitajwa kuwa na majirani
wengi zaidi kwa kuziweka Macau na Hong Kong kama nchi zinazojitegemea
licha ya hini ya mamlaka ya China.
10: Turkey – imepakana na nchi 8
Turkey ina-share eneo la pekee katika
ramani ya dunia, ikiwa na eneo la kilomita za mraba 756,816 Asia
Magharibi (Anatolia) na ardhi ya kilomita za mraba 23,764
Kusini-mashariki ya Europe (Thrace).
Inapakana na nchi nyingi za Europe na
Asia na Bahari Nyeusi upande wa kaskazini, kaskazini-mashariki inapakana
na Armenia na Georgia, mashariki inapakana na Azerbaijan na Iran,
magharibi na kusini-magharibi inapakana na Mediterranean Sea,
kusini-mashariki inapakana na Iran na Syria, na kaskazini-magharibi
inapakana na Ugiriki na Bulgaria.
9: Tanzania – inapakana na nchi 8.
Nchi ya Afrika Mashariki Tanzania ina
majirani wanane zikiwemo nchi za Kenya na Uganda upande wa kaskazini,
Mozambique, Malawi na Zambia upande wa kusini, Rwanda, Burundi na
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo upande wa magharibi.
8: Serbia – inapakana na nchi 8.
Serbia, nchi iliyopo Kusini-mashariki
ya Balkan Peninsula barani Ulaya ni nchi ambayo inapakana na nchi nane
pia. Inapakana na Hungary, Bulgaria, Romania, Macedonia, Montenegro,
Croatia, Bosnia na Herzegovina.
7: Austria – inapakana na nchi nane.
Austria ni nchi inapakana na Jamhuri ya
Czech na kaskazini-mashariki inapakana na Slovakia. Mashariki inapakana
na Hungary na Slovenia upande wa kusini huku Italy ikiwa upande wa
kusini-magharibi. Switzerland na Liechtenstein zipo upande wa magharibi
na Ujerumani upande wa kaskazini-magharibi.
6: Metropolitan France – inapakana na nchi 8.
Ufaransa inapakana na Luxembourg na
Ubelgiji na mashariki inapakana na Italy, Ujerumani na Switzerland,
upande wa kusini inapakana na Uhispania na Andorra na kaskazini
inapakana na England.
5: Ujerumani – inapakana na nchi 9.
Ujerumani inachangia mipaka yake na
nchi 9 ambapo kaskazini inapakana na Denmark, magharibi inapakana na
Netherlands, Luxembourg na Ubelgiji na kusini-magharibi kuna Ufaransa.
Upande wa mpaka wa kusini inapakana na Austria na Switzerland.
Kusiki-mashariki inapakana na Jamhuri ya Czech na mashariki zaidi kuna
nchi ya Poland.
4: DR Congo – inapakana na nchi 9.
Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC)
inapakana na Jamhuri ya Afrika ya Kati, Jamhuri ya Congo, na Sudan.
Mashariki inachangia mpaka na Burundi, Uganda, Tanzania na Rwanda huku
Zambia ikiwa kusini-mashariki na Angola upande wa kusini-magharibi.
3: Brazil – inapakana na nchi 10.
Brazil inachangia mipaka na nchi 10 za
Amerika ya Kusini ambazo ni Argentina, Bolivia, Colombia, Venezuela,
Uruguay, French Guyana, Paraguay, Guyana, Peru, na Suriname.
2: Russia – inapakana na nchi 14.
Ikiwa na mipaka inayofikia urefu wa
kilomita 20,241 Russia ni nchi ya pili kwa kuwa na majirani wengi zaidi
duniani ikipakana na nchi tofauti 14.
Kusini inachangia mipaka na nchi za
Korea Kaskazini, Mongolia na China, Georgia, Kazakhstan, na Azerbaijan
huku kusini-magharibi na magharibi inapakana na Ukraine, Estonia,
Belarus, Latvia, Lithuania, Poland, Norway, na Finland.
1: China – inapakana na nchi 16.
Nchi ya pili kwa ukubwa wa eneo duniani, Jamhuri ya watu wa China
inachangia mipaka ya kimataifa na nchi 16 ikiwemo Korea Kaskazini na
Urusi upande wa kaskazini-mashariki na Mongolia upande wa kaskazini.
Upande wa kusini inapakana na Indian subcontinent inayojumuisha nchi
za India, Bhutan, na Nepal. Vietnam, Laos, na Myanmar ziko upande wa
kusini-mashariki na Pakistan upande wa kusini-magharibi.
Mipaka ya magharibi Afghanistan, Kazakhstan, Kyrgyzstan, na
Tajikistan ambapo mbali na nchi hizi 14 inachangia mpaka na Macau na
Hong Kong.
No comments:
Post a Comment