Mkuu wa Mkoa
wa Dar es salaam Mhe Paul C. Makonda akisikiliza na kujibu maswali ya waandishi
wa habari mapema leo March 30,2017 katika Ukumbi wa Benjamin Mkapa Mjini Dodoma.
|
Baadhi ya
Wakurugenzi wa Manispaa za Jiji La Dar es salaam wakimsikiliza kwa makini Mkuu
wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul C. Makonda wakati akizungumza na Waandishi wa
habari.
|
Waandishi wa
habari wakimsikiliza kwa makini Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul C.
Makonda wakati akielezea ujio wa Waziri Mkuu wa Ethiopia.
|
Mkurugenzi wa
Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo akimsikiliza kwa makini Mkuu wa Mkoa
wa Dar es salaam Mhe Paul C. Makonda wakati akizungumza na waandishi wa habari
kuelezea ujio wa Waziri Mkuu wa Ethiopia katika Ukumbi wa Benjamin Mkapa Mjini
Dodoma.
|
Mkuu wa Mkoa
wa Dar es salaam Mhe Paul C. Makonda akizungumza na waandishi wa habari
kuelezea dhamira ya ujio wa Waziri Mkuu wa Ethiopia nchini Tanzania mapema leo
katika Ukumbi wa Benjamin Mkapa Mjini Dodoma.
Na Mathias
Canal, Dodoma
Waziri Mkuu
wa Ethiopia Mhe Hailemariam Desalegn anataraji kuwasili nchini kesho Machi 31,
2017 katika uwanja wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere kwa ziara ya Siku tatu
kwa kuitikia Mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe
Magufuli ambaye ndiye atakuwa mwenyeji wake.
Taarifa ya
ujio wa waziri Huyo Mkuu wa Ethiopia imetolewa hii Leo na Mkuu wa Mkoa wa Dar
es salaam Mhe Paul C. Makonda wakati akizungumza na waandishi wa habari
kuelezea dhamira ya ujio huo katika Ukumbi wa Benjamin Mkapa Mjini Dodoma.
Rc Makonda
ameeleza kuwa Mhe Desalegn anataraji kuwasili nchini saa tatu kamili asubuhi
Machi 31, 2017 hadi April 1, 2017 ambapo atakuwa nchini kwa shughuli mbalimbali
za kidiplomasia zinazogusa nyanja muhimu za kiuchumi, Biashara, na Ushirikiano
baina ya Nchi ya Ethiopia na Tanzania.
Mhe Makonda
alisema kuwa Waziri huyo Mkuu wa Ethiopia pamoja na shughuli hizo za
kidiplomasia pia atasaini mikataba mitatu, Kutembelea bandari na kufanya
mazungumzo na mwenyeji wake Rais Magufuli.
Makonda
alisema kuwa Tanzania itapata fursa ya kujifunza mambo mengi kupitia kwa ugeni
huo juu ya kukabili changamoto mbalimbali zinazolikabili bara la Afrika katika
masuala ya kilimo cha kisasa katika maeneo yenye uoto wa asili wenye changamoto
kama milima hapa nchini Tanzania.
"Tutajifunza
mengi sana kama ilivyo kwa Ethiopia ambao mbali ya kukabiliwa na uoto usio
rafiki wa milima na miinuko mikali kwa asilimia kubwa bado wameweza kutumia
vyema maeneo machache ya tambarare na Kuwekeza kufanya kilimo cha kisasa na
kuzalisha chakula kwa wingi, hivyo tutapata ufahamu pia katika mambo haya
muhimu" Alisema Mhe Makonda
Kwa niaba ya
wananchi wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe Paul C. Makonda amesema kuwa uongozi wa
Mkoa wake unamkaribisha nchini Tanzania kwani ujio wake utaibua zaidi fursa za
kukuza uchumi na Maendeleo.
Hata hivyo
amesema kuwa Ethiopia imepiga hatua kubwa kwenye usafiri wa Anga Duniani hivyo
kupitia rekodi hiyo nzuri Tanzania pia itapata wasaa wakujifunza mambo mengi
katika sekta hiyo.
|
No comments:
Post a Comment