Akiongea
jana Katika zoezi la uchangiaji damu lililofanyika mjini Kibondo Mkoani Kigoma
kwa kuwahusisha waendesha Pikipiki maarufu Bodaboda, mkufunzi wa mafunzo ya
udereva toka shirika linalojihusisha na utoaji wa mafunzo hayo la APEC, Katema
Kazwika alisema watu wengi mahospitalini wamekuwa wakipoteza maisha kabla
ya wakati kutokana na kukosa huduma ambazo ziko chini ya uwezo wa binadamu.
Kazwika ambae pia alimwakilisha Mkurugenzi
wa shirika hilo ,Respicius Timanywa,
katika kufunga mafunzo ya waendesha pikipiki, alisema kuwa pamoja na kampeni
yao ya uhamasishaji wa wateja wao kujitolea kuchangia Damu, waendesha pikipiki wengi hasa makundi ya
vijana yanakabiliwa na changamoto ya uelewa mdongo wa matumizi ya barabara na
ukosefu wa fedha hali ambayo imekuwa ikisababisha ajali zisizo za lazima na
kwakuwa wahanga wengi wa ajali ni madereva ndiyo maana wamekuwa wakiwashauri kuchangia
damu.
|
Nao baadhi
ya waendesha Bodaboda waliobahatika kuchangia damu amba ni Damasi Lushas na
Emmanuel Kanegene walisema wameamua
kuchangia damu kutokana na adha wanazopata watu mbalimbali mara wanapohitaji
huduma hiyo.
Kwa upande
wake Mteknologia Maabara wa wilaya ya Kibondo, Lina Misanga, alieleseza licha
ya kusaidia wahanga wa ajali damu
imekuwa ni hitaji muhimu katika kusaidia wanawake wajawazito na watoto chini ya
umri wa miaka mitano na kupongeza uamuzi wa wote waliojitolea kuchangia na
kusema ipo changamoto kubwa ya upatikanaji wa damu kwenye hospitali nyingi hapa
nchini, na katika zoezi hilo zimepatikana Unit 25.
Habari/Picha Na-MUHINGO-Kibondo.
|
No comments:
Post a Comment