Wakati mechi
inaelekea ukingoni, Emanuel Martin
aliyeingia akitokea benchi, aliifungia Yanga
SC bao la pili na la ushindi kwa
kichwa alipounganisha pasi ya Musuva
na kumwacha golikipa wa Ruvu Shooting
, Bidii Hussein akiwa hoi baada ya
kujaribu kuufata mpira na kujigonga kwenye nguzo ya goli.
|
Ushindi huo
sasa unaifanya Yanga SC kuendelea kuwa na nafasi ya pili katika msimamo wa Ligi
Kuu msimu huu 2016/2017 kwa kufikisha jumla ya point 52 nyuma ya watani zao
Simba SC wanaoongoza Ligi kwa kuwa na
jumla ya point 54, Ruvu wao bado wapo nafasi ya 10 kwa kuwa na point 28
wakicheza mechi 24, Yanga SC sasa atacheza dhidi ya Mtibwa Sugar siku ya
Jumapili March 05, 2017,katika uwanja wa Jamhuri Morogoro.
Ligi hiyo
ambayo ni michuano mikubwa nchini, itaendelea mwishoni mwa wiki hii ambako kwa
siku ya Jumamosi Machi 04, mwaka huu 2017, Simba SC itacheza na Mbeya City kwenye Uwanja
wa Taifa, Dar es Salaam.
Azam FC pia
itacheza Jumamosi Machi 04, mwaka huu na Stand United ya Shinyanga kwenye Uwanja
wa Chamazi. Mchezo huo utaanza saa 1.00 jioni wakati mechi nyingine zitaanza
saa 10.00 jioni.
Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limerejesha tena mechi za Ligi Kuu kwenye
Uwanja wa Jamhuri, Morogoro na Jumapili Machi 05, mwaka huu Mtibwa Sugar
itaialika Young Africans kwenye uwanja huo katika mfululizo wa mechi za Ligi
Kuu ya Vodacom Tanzania Bara.
Mchezo
mwingine wa Ligi Kuu ya Vodacom utachezwa Uwanja wa Uhuru ambako African Lyon
itaialika Mwadui FC ya Shinyanga wakati Ndanda FC itakuwa mwenyeji wa Ruvu
Shooting kwenye Uwanja wa Nangwanda Sijaona.
|
No comments:
Post a Comment