Mkuu wa
wilaya ya Geita ,mkoani Geita,Bw.Herman Kapufi ameteketeza na kuvuruga shamba la Bangi ambalo linasadikika kuwa na ukubwa wa hekari
mbili na nusu la Bangi huku akisisitiza kuwa
hakuna mtu yoyote atakeyepona
ndani ya Wilaya yake iwapo atabainika anajihusisha na madawa ya
kulevya ambayo yamekuwa ni hatari kwa
vijana wengi.
Mkuu huyo wa
Wilaya alitoa kauli hiyo jana wakati wa zoezi la kuteketeza kwa moto mimea ya bangi kwenye shamba ambalo lipo
Mtaa wa Samina B kata ya Mtakuja iliyopo halmashauri ya Mji wa Geita.
Bw.Kapufi
alisema vijana wengi wanaokaa kwenye
vijiwe wanaangamia kwa uvutaji wa bangi na kwamba watu wanaojishughulisha na
ulimaji pamoja na usambazaji hatasita kuwachulia hatua kali za kisheria, huku
akitoa rai kwa wananchi kuwafichua wanaojihusisha na biashara hiyo haramu.
|
Bangi ambayo
ilikuwa imekwisha kukomaa kwaajili ya kuuzwa ikioneshwa kwa Mwenyekiti wa
kamati ya ulinzi na usalama.
|
‘’Ndani ya
Wilaya yangu sitasita kuwachulia hatua watu wote wanaojihusisha na ulimaji
ikiwemo usambazaji wa madawa ya kulevya
hatuwezi kuona vijana ambao ni nguvu kazi ya taifa wakiteketea kwa
madawa hatutakubali…lakini niwashukuru wananchi waliotupatia taarifa kuwepo kwa
shamba hili ambalo leo [jana] tunachoma motomimea ya bangi’’alisema Kapufi.
kwa upande
wake Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa wa samina B. John Balenge alisema kuwa
walipata taarifa za shamba hilo la bangi kutoka kwa wananchi waliokuwa wakienda
porini kufanya shughuli za kutafuta kuni na mkaa na kwamba waliweka mtego wa
kumnasa mwenye shamba bila mafanikio.
‘’Ndugu
waandishi kama mnavyoona shamba hili linaonesha mwenye nalo alikuwa akilitunza
limesafishwa vizuri niseme tu sisi tulipata taarifa kwa wananchi tukawa
tunaweka ulinzi wa kumkamata mmiliki ni mwezi sasa bila mafanikio,’’alisema
Mwenyekiti huyo.
|
Naye diwani
wa kata ya Mtakuja ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa halmashauri ya Mji wa Geita,
Constatine Morand alisema hayuko
tayari kumuona mtu akifanya biashara ya madawa ya kulevya katika kata yake na
kwamba wanamuunga mkono rais katika vita hiyo.
‘’Nitowe wito kwa wananchi wote wa kata ya
Mtakuja siko tayari kuona biashara hii ikiendelea kwenye kata yanngu na
kuangamiza watanzania wengi…na sisi huku chini tunamuunga mkono rais wetu Dk.
John Magufuli katika vita hii waliyoianzisha,’’alisema Morandi.
|
Akizungumza
na Wana Habari, mmoja katti ya vijana ambao walikuwa wakitumia Bangi hapo
zamani na kuamua kuachana nazo ,Juma Suleiman alisema madawa hayo ya kulevya
hayana faida yoyote na badala yake yanatia hasara kwa vijana na kurudisha
maendeleo nyuma.
Kutokana na
biashara hii ya bangi kushamiri katika
visiwa vilivyoko mwambao wa ziwa victoria, Mkuu wa Wilaya alisema wakimaliza
oparesheni maeneo ya nchi kavu watahamishia nguvu majini kwenda kupambana na
wafanyabiashara wa zaohilo haramu.
IMEANDALIWA
NA MADUKA ONLINE
|
Kamati ya
ulinzi na usalama wilayani Geita haikuwa nyumba katika shughuli hiyo.
|
Mkurugenzi
wa Halmashauri ya wilaya ya Geita,Ali Kidwaka akishughulika.
|
Shughuli ya
uondoaji wa Bangi ikiendelea Mkurugenzi wa Mji wa Geita ambaye amevaa Mkoti wa suti Mhandisi Modest
Aporinaly akigoa moja kati ya mmea wa Bangi.
|
Mkuu wa
wilaya ya Geita,akiteta jambo na baadhi ya wananchi na mwenyekiti wa mtaa
pamoja na diwani wa kata ya Mtakuja kabla ya zoezi la kuondoa zao hilo.
|
Mkuu wa
Wilaya ya Geita ,Mwl Herman Kapufi akikagua na kuangalia namna ambavyo shamba
hilo limelimwa.
|
No comments:
Post a Comment