Wizara ya
Mambo ya Ndani, kupitia Jeshi la Polisi, na vyombo vingine vya ulinzi na
usalama, itashiriki katika operesheni, ikiwemo kwenye masuala ya inteligensia.
Ofisi ya
Makamu wa Rais na Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira,
wataratibu operesheni.
Kama tangazo
letu la tarehe 20/2/2017 lilivyoonesha muda wa nyongeza unaweza kutolewa kwa
wazalishaji halali ambao wataonyesha ushahidi wa kuelekea kuhamia kwenye
teknolojia ya chupa, na kwamba watahitaji muda mchache kufanya hivyo, na ambao
watatimiza masharti kadhaa na kupata kibali maalum kabla ya tarehe
28/2/2017.
Hadi sasa Serikali imepokea maombi ya wazalishaji 9. Tutangaza kesho iwapo kuna ambao wamekidhi masharti au la. Kanuni za upigaji marufuku pombe hizi zipo tayari.
Pia
tumepokea malalamiko kwa wazalishaji wengi kwamba zoezi hili limekuja ghafla na
wengine wana malighafi na bidhaa kwenye maghala. Ukweli ni kwamba Serikali
ilitoa taarifa Bungeni, kuanzia mwezi Mei 2016, na mara kadhaa baada ya hapo,
na rekodi zipo, kuhusu hatua hizi.
Vilevile, taarifa ya Serikali iliyotangaza kupiga marufuku pombe za viroba ziliripotiwa kwa ukubwa stahiki kwenye vyombo vya habari, ikiwemo kwenye ukurasa wa kwanza wa gazeti la Mwananchi, mwezi Agosti 2016. Katika taarifa zote za nyuma, Serikali ilitangaza kwamba hatua hiyo itaanza tarehe 1 Januari 2017. Hatua hizi zimechelewa kwa miezi miwili. Iwapo, baada ya taarifa hizo za Serikali, kuna mzalishaji ameagiza malighafi au kutengeneza au kuhifadhi pombe za viroba, au kuchukua mkopo kwa ajili hiyo, atakuwa amefanya hivyo akijua madhara yake.
Mwisho
napenda kutoa wito kwa wananchi wote kutoa ushirikiano katika utekelezaji wa
zoezi hili la upigaji marufuku matumizi ya pombe zinazofungashwa katika
vifungashio vya plastiki (viroba) kwa kutoa taarifa kwa vyombo husika ili wale
wanaozalisha na kuuza au kuhifadhi waweze kuchukuliwa hatua stahiki. Zawadi
itatolewa kwa watakaotoa taarifa zitakazowezesha kukamatwa kwa watakaokiuka
zuio hili.
OFISI YA
MAKAMU WA RAIS
28/02/2017.
|
Wednesday, March 01, 2017
VIROBA: Marufuku Kuanzia Leo,Kuanzia Machi 02,2017 Ukikutwa Utakiona.
Tags
# HABARI
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
HABARI
Labels:
HABARI
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment