Amesema
amemwagiza mkuu wa jeshi la polisi kutumia picha zilizopigwa wakati wa tukio
hilo kumsaka mhusika.
"Nape
Moses Nnauye sio jambazi, ni Mtanzania, ni mbunge, mjumbe wa NEC wa CCM, hana
rekodi ya uhalifu. Kitendo cha mtu kumtolea bastola, sio cha kiasikari, sio cha
Kitanzania na sio cha ki Mungu, kama mtu ameweza kutoa bastola mbele ya kamera
nawaza mbali ingekuwa kwenye uchochoro angefanya nini," ameandika.
"Nahusika
na usalama wa raia wote wa Tanzania, nimemwelekeza IGP atumie picha kumsaka mtu
yule aliyeinua kufanya kitu cha kihalifu kwa kofia ya uaskari. Na kama ni
askari basi sheria zinazoongoza taasisi husika zichukue mkondo wake.
|
Katika hatua
nyingine, Aliyekuwa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Nape Nnauye amewashukuru waandishi wa
habari kwa mchango wao pamoja na upendo waliomuonyesha wakati wa uwaziri wake.
Mbunge huyo
wa jimbo la Mtama, amesema hayo kupitia Twitter:
..Wanahabari
mme GUSA sana moyo wangu!Sikujua kama mnanipenda na kunithamini kiasi
KILE!Nawashukuru SANA kwa kujitolea kwenu!Nawapenda SANA!
|
No comments:
Post a Comment