Serikali ya
Tanzania imezindua Ujenzi wa mradi wa kufua umeme katika maporomoko ya Rusumo yaliyopo
wilayani Ngara mkoani Kagera ,utakaonufaisha nchi 3 za Tanzania,Rwanda na
Burundi hapo Jana March 30,2017.
Uzinduzi wa
mradi huo utakaogharimu dola za Kimarekani 340 milioni ,umeshuhudiwa na
Mawaziri wa Nishati kutoka nchi hizo tatu sambamba na wafadhili kutoka Benki ya
Dunia.
Mradi huo
unatarajiwa kukamilika Februari 2020 na kuzalisha megawati 80,huku kila nchi
ikipata mgawanyo wa zaidi ya megawati
20.
|
Waziri wa
Nishati na Madini wa Tanzania ,Profesa Sospeter Muhongo amesema mradi huo
unafadhiliwa na Benki ya Dunia ambapo kwa upande wa Tanzania itachangia kwa
asilimia mia moja.
Waziri
Muhongo amebainisha kwamba ,kwa upande wa nchi ya Burundi haitachangia gharama yoyote katika mradi huo huku nchi ya Rwanda
ikichangia asilimia 50.
|
Ni kikundi cha wasanii kutoka Rwanda. |
Burudani ikiendelea wakati wa uzinduzi huo-Ni kikundi cha wasanii kutoka Burundi.
Mwakilishi
kutoka Benki ya Dunia ,Bw.Bella Bird amesema ni miongoni mwa miradi
iliyowavutia ya uzalishaji wa umeme katika maporomoko ya Rusumo na hawakusita
kuwekeza katika eneo hilo.
Amesema
mradi huo utasaidia kuwepo kwa uhakika wa umeme katika ukanda huo na kusaidia
maendeleo ya kiuchumi na kijamii kwa wananchi wa nchi hizo.
Amesema
mradi huo ukikamilika utapunguza mahitaji ya nishati hiyo na kufungua nafasi za
ajira na kuwa Benki ya Dunia inaona kuna faida nyingi huku akisisitiza Mkandarasi
wa Mradi huo kukamilisha kazi hiyo kwa mujibu wa makubaliano.
|
No comments:
Post a Comment