Timu ya
taifa ya mpira wa miguu ya vijana wenye umri wa miaka 17, Serengeti Boys
imeondoka kwenda mkoani Kagera wameenda na ndege ya (ATCL) kutoka Dar es
Salaam, alfajiri ya Machi 26, mwaka huu kwa kambi ya wiki moja.
Serengeti
Boys itakuwa kambini Bukoba hadi Aprili 02, mwaka huu,2017 ambako inatarajiwa
kucheza michezo miwili ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya timu vijana ya Burundi
kwenye Uwanja wa Kaitaba, mjini Bukoba mkoani Kagera. Michezo hiyo itafanyika
Machi 30, 2017 na kurudiana Aprili mosi, mwaka huu.
Serengeti
Boys ambayo inajiandaa na michuano Afrika huko Gabon itarejea Dar es Salaam
Aprili 2, mwaka huu ambako imepangwa kucheza na Ghana Aprili 3, mwaka huu
kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Mchezo huo utatanguliwa na hafla ya
kuagwa kwa kukabidhiwa bendera.
Timu
itaelekea Morocco Mei 5, mwaka huu baadaye itapita Cameroon kwenye kambi ya
zaidi ya mwezi mmoja baadaye itakwenda Gabon katika michuano itakayoanza Mei
14, 2017. Ikiwa Cameroon itacheza mechi mbili za kimataifa dhidi ya wenyeji
kabla ya kwenda kwenye fainali.
Serengeti
Boys ni timu ya vijana ambayo imefuzu kwa fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika
zitakazofanyika Gabon kuanzia Mei 14, mwaka huu. Timu hiyo imepangwa Kundi ‘B’
pamoja na mabingwa watetezi Mali, Niger na Angola. Ina lengo la kurejea na
Kombe la Afrika kwa vijana.
La ikitokea
imekosa nafasi hiyo angalau ikafika nusu fainali ambako kwa mafanikio hayo
itakuwa tayari ina tiketi mkononi ya kucheza fainali za Kombe la Dunia huko
India, Novemba, mwaka huu,2017.
Kikosi cha
Serengeti Boys kinaundwa na Makipa:-
Ramadhan Kabwili
Samwel Edward
na Kelvin
Kayego.
Walinzi:-
Kibwana Ally Shomari
Nickson Kibabage
Israel Mwenda
Dickson Job
Ally
Msengi
Issa Makamba
na Enrick Vitalis Nkosi.
Viungo:-
Kelvin Nashon Naftali
Ally Ng’anzi
Mohamed Rashid
Shaaban Ada
Mathias Juan
Marco Gerald
Abdulhamis Suleiman
Saidi Mussa
na Cyprian Benedictor Mtesigwa.
Washambuliaji:-
Muhsin Malima Makame
Yohana Mkomola
Ibrahim Abdallah
Assad Juma
na Abdul
Suleiman.
Benchi la
Ufundi:-
Bakari Shime
(Kocha Mkuu)
Oscar
Mirambo (Kocha Msaidizi)
Muharami
Mohamed (Kocha wa makipa)
Kim Poulsen
(Mshauri wa Ufundi)
Edward Evans
(Mtunza Vifaa)
Shecky
Mngazija (Daktari wa timu)
|
No comments:
Post a Comment