Mwenyekiti
wa Taasisi hiyo, Jakaya Kikwete, alisema kuwa Taasisi hiyo pamoja na mambo
mengine itajihusisha na masuala ya
Maendeleo ya Binadamu nchini, Afrika na Duniani.
|
Kikwete
akizungumza na baadhi ya wajumbe wa Bodi ya Wadhamini wa Taasisi yake ya JMKF.
|
Jakaya
Kikwete akikumbatiana na Mjumbe wa Bodi ya Wadhamini wa Taasisi hiyo, Balozi wa
zamani wa Marekani nchini Tanzania, Charles Stith.
|
Dato' Sri Idris Jala kutoka Malaysia.
Genevieve Sangudi kutoka Marekani
Mwanasheria Maarufu nchini, Balozi Mwanaidi Sinare Maajar. Alikuwa Balozi wa Tanzania nchini Uingereza 2006 na Marekani 2013
Daktari Bingwa wa Upasuasi, Profesa Wiliam Mahalu
Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Rwekaza Mukandara
Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi la Makampuni la SS Bakhresa, Abubakar Bakhresa
Balozi wa zamani wa Marekani nchini, Charles Stith
Na
Immaculate Makilika- MAELEZO.
Rais Mstaafu
Dk. Jakaya Kikwete amezindua Taaisi yake ya kusaidia jamii, nakusema ameamua
kuanzisha taaisi hiyo ili kuwa na chombo kitakachomsaidia kuendeleza maono yake
ya kutimiza ndoto zake katika kuendelea kusaidia jamii.
Akizindua
taasisi hiyo yenye jila la Jakaya Mrisho Kikwete Foundation, Kikwete amesema,
kwa muda mrefu amekua akipenda na kujihusisha na shughuli mbalimbali za
maendeleo ya watu na hivyo taasisi yake itamsaidia katika kufikia malengo yake.
“Nimetumia
muda wangu kwa ajili ya maendeleo ya watu, baada ya shule, nilikitumikia Chama
cha Mapinduzi (CCM), nilitumikia Jeshi na baadae Serikali, kwangu Taasisi hii
imekuwa chombo kitakachonisaidia kuendeleza maono yangu na kutimiza ndoto zangu
katika kuendelea kusaidia watu” alisema Dk. Kikwete.
Akizungumzia
taasisi hiyo Kikwete amesema ni taasisi yenye wajumbe tisa kutoka sehemu
mbalimbali duniani wenye nyadhifa na heshima kubwa katika nchi zao.
Dk. Kikwete
amewataja Wajumbe wa Bodi ya Udhamini ya Taasisi yake kuwa ni Balozi Ombeni
Sefue aliyekuwa Katibu Mkuu Kiongozi, Profesa Rwekaza Mukandala, Makamu Mkuu wa
Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM), Profesa Willium Mahalu Mhadhiri
Mwandamizi katika Chuo Kikuu cha Tabibu
cha Bugando.
Wengine ni
Balozi Mwanaidi Maajar aliyewahi kuwa Balozi wa Tanzania nchini Uingereza,
Abubakar Bakhresa, Mkurugenzi Mtendaji wa Kundi la Makampuni ya Bakhresa,
Genevieve Sangudi Mtaalamu wa Masuala ya
kibishara ya Kimataifa kutoka Marekani.
Aliwataja wengine kuwa ni Dato’ Sri Idris Jala, Waziri asiyekuwa na Wizara
Maalumu nchini Malyasia, Balozi Charles
R. Stith aliyekuwa Balozi wa zamani wa Marekani nchini Tanzania pamoja na Dkt.
Carlos Lopes ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taaisi ya Mafunzo na Utafiti ya Umoja
wa Mataifa (UNITAR).
Amesema
taasisi hiyo inajikita kusaidia jamii katika maeneo makubwa manne ya maendeleo
ya jamii ikiwemo kuondoa umaskini,
mabadiliko ya tabia nchi, kilimo kwa
wakulima wadogo, huduma za afya ikiwemo kutokomeza malaria na afya ya mama na
mtoto.
Maeneo
mengine ameyataja taasisi hiyo kushughulika nayo ni elimu kwa vijana ili
kukuza vipaji vyao na kuwapa mafunzo kuhusu uongozi bora, usawa wa
kijinsia na namna ambavyo Serikali inavyotoa huduma kwa wananchi.
Amesisitiza
kuwa taasisi yake itaisaidia Serikali, mashirika na taasisi mbalimbali ili
kushirikiana kuwaletea maendeleo Watanzania na watu mbalimbali duniani.
Taasisi ya
Maendeleo ya Jakaya Kikwete ilisajiliwa tarehe 17, Februari 2017, na hii ni
mara ya kwanza kwa wajumbe wa bodi ya wadhamini kukutana tangu kuanzishwa
kwake.
No comments:
Post a Comment