Tawi hilo
linawanachama 60 walio hai na wanaosubiri kukabidhiwa Kadi za Uanachama na
Uongozi wa Klabu ya Simba SC huku wengine 160
wakiwa tayari nao wamekamilisha taratibu za kuwa wanachama hai.
|
Mwenyekiti
wa Muda wa Tawi hilo Prisius Massai maarufu kwa jina la Majeshi amesema
uzinduzi wa tawi hilo umeenda sambamba na ufunguzi wa Ofisi katika eneo la
Hamgembe mjini Bukoba ikiwa ni hatua yao ya kuiunga mkono Klabu ya Simba SC yenye makao makuu yake Jijini Dar Es Salaam.
Massai
anasema pamoja na kuhamasisha wapenzi wa Simba SC mkoani Kagera kujiunga katika
Tawi lao ili kukuza mahusiano na wanatarajia umoja huo uwanufaishe kwa kupanua
wigo kwa kutoka kwenye ulipaji wa ada ya mwaka na kufungua mfuko wa Tawi au
SACCOS ili kuwasaidia wanachama
kuleteana uchumi na maendeleo.
|
Tawi hilo la
Wanachama wa Simba SC Manispaa ya Bukoba mkoani Kigoma limepewa Jina la
KICHWABUTA ikiwa ni kuenzi Kazi kwa Vitendo ya Marehemu Mzee Omary Hussein
Kichwabuta ambaye alikua ni Mwanachama na Shabiki mkubwa wa Simba SC.
|
No comments:
Post a Comment