Mwanamuziki wa
Bongofleva Nchini Tanzania, Emmanuel Elibariki maarufu Nay wa Mitego amekamatwa
na Polisi leo March26,2017,majira ya asubuhi mkoani Morogoro na kupelekwa katika
Kituo cha Polisi Mvomero mkoani humo.
Nay wa
Mitego amekamatwa akiwa hotelini Morogoro baada ya kuamaliza shughuli zake
zilizompeleka ambapo alitakiwa kuongozana na polisi hao hadi kituo cha polisi.
Nay
ameandika kwenye Instagram yake “.....
|
“Nimekamatwa
kweli. Muda Huu nikiwa hotel Morogoro baada ya kumaliza Kazi yangu iliyo ni
leta. Napelekwa Mvomelo Police. Nawapenda Watanzania wote. ✊🏿✊🏿 #Truth #Wapo.” Ameandika Nay wa
Mitego kupitia ukurasa wake wa Instagram.
Licha ya
kuwa Mwanamuziki huyo hajaeleza sababu ya kukamatwa kwake, au Jeshi la Polisi
kutoa taarifa, lakini inaaminika kuwa sababu kubwa ni wimbo wake alioutoa siku
za hivi karibuni unaokwenda kwa jina la Wapo.
Wimbo huo
umezungumzia mambo mengi hasa ya kisiasa yanayoendelea nchini kwa sasa ikiwa ni
pamoja na tuhuma zinazomkabili Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda,
uhuru wa vyombo vya habari na masuala ya
sanaa.
|
No comments:
Post a Comment