Mratibu Miradi wa Taasisi wa MO Dewji,
Catherine Decker akizungumza kuhusu ushirikiano wa MO Dewji Foundation na Tulia
Trust kujenga vyoo katika wodi ya wanawake katika Hospitali ya Rungwe.
“Huduma za afya ya uzazi zimekua ni
changamoto katika sekta ya afya nchini, hivyo taasisi yetu imekusudia kutoa
misaada ili kuziboresha na sasa safari yetu imetuleta mkoani Mbeya, ambapo tuna
muunga mkono Mheshimiwa Naibu Spika kuchimba vyoo katika hospitali ya Rungwe
kwenye wodi za kina mama wajawazito,
“Wanawake ni msingi wa maendeleo katika jamii
zetu, tafiti zinaonyesha kuwa kufanya kazi na wanawake, kunawapa nafasi ya
kuongeza kipato chao, kwani ni njia bora katika kuchangia maendeleo chanya kwa
jamii,” alisema Catherine na
kuongeza.
“Lakini ili tuwaheshimu wanawake tunapaswa
kuhakikisha kuwa wanapata huduma za afya ya uzazi, ikiwemo vifaa bora pamoja na
mazingira safi ili kuboresha usalama wa afya zao. Kwa kufanya hivi itachangia
kuboresha sekta ya afya katika jamii zetu, jambo ambalo tuna litazamia kama
taasisi.”
Kwa upande
wa Naibu Spika wa Bunge la Tanzania na mwanzilishi wa Taasisi ya Tulia Trust,
Dk. Tulia Ackson aliishukuru Taasisi ya
Mo Dewji kwa udhamini huo ambao umeambatana na mashindano ya kukimbia ya Tulia
Marathon na malengo ya kuanzisha mashindano hayo ni kukusanya pesa ili kusaidia
kuboresha sekta ya elimu na afya.
|
Naibu Spika wa Bunge la Tanzania na
mwanzilishi wa Taasisi ya Tulia Trust, Dk. Tulia Ackson akizungumza kuhusu
ushirikiano wa MO Dewji Foundation na Tulia Trust kujenga vyoo katika wodi ya
wanawake katika Hospitali ya Rungwe.
“Tulikuwa na malengo maalumu ila kikubwa ni
kuimarisha afya na elimu, hospitali ya Rungwe kwa sasa wodi ya kina mama ina
choo kimoja na sisi kama Tulia Trust kwa kushirikiana na wadhamini wetu [Mo
Dewji Foundation] tumepata fedha ambazo tutajenga vyoo kwa ajili ya hiyo wodi
ya kina mama na mabafu pia,
“Na hicho ndicho kinachotofautisha marathon
hii ya kwetu na hizo zingine, hii tulikuwa na mpango maalumu wa kukusanya fedha
ili tuweze kuboresha miundombinu ya elimu na afya na huu ni mwanzo tu mwakani
tutafanya mambo mengi zaidi,” alisema Dk.
Tulia.
|
No comments:
Post a Comment