Kibondo na Changamoto la Ongezeko la Maambukizi ya UKIMWI kwa asilimia 1.9 sasa. - Mwana Wa Makonda

Muhtasari

X-BET


Post Top Ad

Sunday, March 05, 2017

Kibondo na Changamoto la Ongezeko la Maambukizi ya UKIMWI kwa asilimia 1.9 sasa.

Kutokana na ujio wa wakimbizi toka nchini Burundi na kuongezeka idadi ya watu wanofika kufanyakazi  katika mashirika ya kuhudumia wakimzi wilayani Kibondo mkoani Kigoma imedaiwa kuwa ni chanzo cha ongezeko la maambukizi ya Virus vya ukimwi.

 Inadaiwa  Mabinti wengi wameanza kutoka maeneo ya vijijini na kujikusanya kwenye madangulo kwa ajili ya kujiuza kutokana na msongamano wa watu kuwa wengi na wenye tabia tofauti kwa ajili ya kutafuta pesa

Kutokana na hali hiyo, kwenye kikao cha baraza la madiwani wa halmashauri hiyo kilichoketi Juzi, Hadija Maulid na Fales Nzobona, wameitaka serikali kupiga marufuku na kusambaratisha maeneo yote yanayojihusisha na biasha ya matendo ya Ngono yakiwemo Madangulo na uvaaji wa mavazi yanayosadikiwa kuchoe hali hiyo kwa wanawake na wasichana

'' Inashangaza wasichana kuvaa mavazi ya ajabu na wanatoroka vijijini kuja mjini pia wapo baadhi ya viongozi wa Dini wanao wapotosha wananchi kula vyakula vya aina flani ili watakapopimwa ugonjwa usionekane hali hii ni ni hatari sana kama itaachiliwa na kuendelea alisema Nzobona

Mratibu wa kitengo cha ukimwi kibondo Elizabet Ntabandi amekiri kuwepo kwa ongezeko la maambukizi kuwa awali yalikuwa asilimia 0.7 na sasa yako asilimia 1.9 na kusema kuwa wanaendelea kuwaelimisha wananchi na kugawa mipira katika Vilabu vya pombe na nyumba za kulala wageni

Pamoja na mambo mengine katika kikao hicho cha baraza la madiwani wameendelea kulalamikia Idara ya ardhi kipitia maliasili kuchelewa kutoa hati miliki za kudumu kwa makazi ya wananchi vijini ili majengo na ardhi zao ziweze kumilikiwa kihalali kwa kuwa ni agizo la serikali huku afisa amaliasili Fred Eliasafu akieleza kuwa tatizo lilikuwa katika ofisi za ardhi mkoa wa kigoma kwakuwa afisa ardi mteule alihamishwa na sasa ameletwa mwingine hivyo baada ya miezi mitatu zitakuwa tayari.

''Hati hizo kwa mujibu wa sheria zinasainiwa na Afisa ardhi mteule wa mkoa hivyo aliyekuwepo alihamia Dsalam na kwa kuwa ameletwa mpya tutalifanyia kazi maana tulimuhusisha alisema anasaini za Wilaya ya Kasulu na akimaliza atanza za kwetu alisema Eliasafu''

Pamoja na kuahidiwa kuwa tatizo hilo kumalizika baada ya miezi mitatu mwenyekiti wa halmashauri hiyo Simon Kanguye amesema kumekuwepo na watendaji wengi kutotekeleza mambo kwa wakati hali inayosababisha  malaumu kwa wananchi na kukosa imani na viongozi wao baada ya kusikia kauli zao.

Picha/Habari na-Muhingo/Kibondo.

No comments:

Post a Comment

Post Bottom Ad