''
Inashangaza wasichana kuvaa mavazi ya ajabu na wanatoroka vijijini kuja mjini
pia wapo baadhi ya viongozi wa Dini wanao wapotosha wananchi kula vyakula vya
aina flani ili watakapopimwa ugonjwa usionekane hali hii ni ni hatari sana kama
itaachiliwa na kuendelea alisema Nzobona
Mratibu wa
kitengo cha ukimwi kibondo Elizabet Ntabandi amekiri kuwepo kwa ongezeko la
maambukizi kuwa awali yalikuwa asilimia 0.7 na sasa yako asilimia 1.9 na kusema
kuwa wanaendelea kuwaelimisha wananchi na kugawa mipira katika Vilabu vya pombe
na nyumba za kulala wageni
Pamoja na
mambo mengine katika kikao hicho cha baraza la madiwani wameendelea kulalamikia
Idara ya ardhi kipitia maliasili kuchelewa kutoa hati miliki za kudumu kwa
makazi ya wananchi vijini ili majengo na ardhi zao ziweze kumilikiwa kihalali
kwa kuwa ni agizo la serikali huku afisa amaliasili Fred Eliasafu akieleza kuwa
tatizo lilikuwa katika ofisi za ardhi mkoa wa kigoma kwakuwa afisa ardi mteule
alihamishwa na sasa ameletwa mwingine hivyo baada ya miezi mitatu zitakuwa
tayari.
|
''Hati hizo
kwa mujibu wa sheria zinasainiwa na Afisa ardhi mteule wa mkoa hivyo
aliyekuwepo alihamia Dsalam na kwa kuwa ameletwa mpya tutalifanyia kazi maana
tulimuhusisha alisema anasaini za Wilaya ya Kasulu na akimaliza atanza za
kwetu alisema Eliasafu''
Pamoja na
kuahidiwa kuwa tatizo hilo kumalizika baada ya miezi mitatu mwenyekiti wa
halmashauri hiyo Simon Kanguye amesema kumekuwepo na watendaji wengi
kutotekeleza mambo kwa wakati hali inayosababisha malaumu kwa wananchi na kukosa imani na
viongozi wao baada ya kusikia kauli zao.
Picha/Habari na-Muhingo/Kibondo.
|
No comments:
Post a Comment