Nchi ya Kenya imesoma Bajeti yake ya mwaka 2017/2018, hapo Jana March 30,2017 kinyume na inavyosomwa kawaida mwezi
Juni, kutokana na Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Agosti mwaka huu 2017, huku ikitangaza
kusimamisha ajira katika sekta ya umma.
Katika
Bajeti hiyo ya shilingi za Kenya Trilioni 2.6 (Takriban shilingi trilioni 52 za
Tanzania) ambapo Waziri wa Fedha wa nchi hiyo, Mhe.Henry Rotich ameondoa kodi kwenye
mahindi yanayoagizwa kutoka nje kwa kipindi cha miezi minne ijayo,
Aidha kodi
imeondolewa kwenye dawa za kuulia wadudu za nchini humo pamoja na magari ya
utalii yanayoundwa nchini Kenya.
Katika bajeti
hiyo ambayo ni ya mwisho kwa serikali ya Jubilee katika muhula wake wa kwanza,
serikali imeongeza kodi kwenye kamari hadi 50% kutoka 7.5% ya awali kama njia
ya kukomesha uchezaji kamari.
Serikali pia
imetangaza kusimamisha ajira katika sekta za umma isipokuwa sekta ya elimu kama
njia ya kupunguza matumizi.
Jumla ya
Shilingi bilioni 524.6 za kenya katika Bajeti hiyo zitatokana na mikopo kutoka
nje na ndani ya nchi.
Shilingi
bilioni 2 za Kenya zimetengwa kuwaajiri
walimu, na zingine bilioni 4 kuwalipia mtihani wanafunzi wa darasa la nane na
kidato cha nnemwaka 2017 na 2018 huku serikali za kaunti zikipata jumla la
shilingi bilioni 329.
Ili
kuhakikisha kuwa vijana wana ajira, serikali imetenga shilingi milioni 450 Ksh
kwa kuboresha kiwanda cha Rivatex, na zingine milioni 250 kuboresha kiwanda cha
Maziwa cha New KCC.
|
No comments:
Post a Comment