Bui bui hula
zaidi ya tani milioni 400 za wadudu kila mwaka duniani .
Matokeo hayo
yamechapishwa katika nakala ya Science of Nature.
Dr Martin
Nyffeler kutoka cho cha sayansi cha Basel ambaye aliongoza utafiti huo,
alichochewa na kitabu cha mwaka 1958, kinachofahamika kama dunia ya buibui,
ambapo mwanasayansi raia wa Uingereza anadai kuwa uzito wa wadudu wanaouawa
kila mwaka na buibui nchini Uingerzea, ilizidi uzito wa watu wote nchini humo.
Baada ya
miongo minne ya kukusanya takwimu, alipata taarifa za kutosha kuweza kubaini ni
kiwamgo kipi cha chakula buibui wanakula.
Dr Nyffeler
anasema kwa bui bui wote duniani ambao ni wana uzito wa tani milioni 25,
wanawinda na kula kati ya tani milioni 400 na 800 za wadudu kila mwaka.
Sasa
wanasayansi wanasema kuwa utafiti huo utatoa hamasisho kuhusu umuhimu kwa
buibui duniani.
"Buibui
huua na kula idadi kubwa ya wadudu waharibifu, na kwa kufanya hivyo hulinda
mimea wasiharibiwe," alisema Dr Nyffeler.
|
Wednesday, March 15, 2017
Fahamu:Buibui hula zaidi ya tani milioni 400 za Wadudu kila Mwaka Duniani.
Tags
# DONDOO
Sambaza Hii
Chief Editor | Mhariri
DONDOO
Labels:
DONDOO
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kuhusu Mwandishi
Journalist / Chief Editor / Tanzanian Blogger
Simu: 0756830214 / 0620197747 / 0789925630.
No comments:
Post a Comment