Aliyekuwa
rais wa Misri, Hosni Mubarak ameripotiwa kuachiliwa huru baada ya kukaa jela
kufuatia maandamano yaliomng’atua mamlakani 2011.
Bwana
Mubarak alikuwa akizuiliwa katika hospitali ya kijeshi mjini Cairo, lakini
wakili wake aliiambia BBC kwamba sasa ameruhusiwa kurudi nyumbani kwake mjini
humo.
Aliagizwa
kuachiliwa huru mapema mwezi huu baada ya mahakama ya rufaa kumuondolea makosa
ya kuwaua waandamanaji wakati wa maandamano dhidi yake 2011.
Bwana
Mubarak mwenye umri wa miaka 88 alichukua mamlaka 1981 baada ya mauaji ya
aliyekuwa kiongozi wa taifa hilo Anwar Sadat.
Amekuwa
akizuiliwa katika hospitali ya kijeshi ya Maadi tangu 2013 baada ya kuhamishwa
katika eneo hilo kwa dhamana kutoka jela ya Torah.
Mubarak
alihukumiwa kifungo cha maisha baada ya kupatikana na hatia 2012 ya mauaji ya
waandamanaji waliouawa katika mikono ya vikosi vya usalama mnamo mwezi Februari
2011.
Kesi
nyengine ilianzishwa na jaji akaamuru kwamba Mubaraka anaweza kutolewa mwezi
Mei 2015.
Hatahivyo
serikali ya rais Abdul Fattah al-Sisi iliripotiwa kwamba haipo tayari
kumuachilia huru kutokana na upinzani ambao huenda ungejitokeza miongoni mwa
raia iwapo ataachiliwa.
Bwana Sisi
alihudumu kama mkuu wa kitengo cha ujasusi cha rais Mubarak katika jeshi na
aliongoza jeshi kumuondoa madarakani mrithi wa Mubarak, Mohammed Morsi 2013.
|
No comments:
Post a Comment