Timu ya
Taifa ya Brazil imekuwa Nchi ya
Kwanza kufuzu kwenda kwenye Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2018 huko Nchini
Russia huku wakiwa wamebakiza Mechi
4 za Kundi lao la Nchi 10 za Marekani ya Kusini.
Uhakika wa
hili umetimia hii Leo March 29, 2017 baada ya Brazil kuwachapa Paraguay
3-0 na Uruguay kufungwa 2-1 na Peru katika Mechi ya mwisho iliyochezwa
Alfajiri ya Leo.
Sasa Brazil wanaungana na Wenyeji wa Fainali
za Kombe la Dunia za Mwaka 2018 -Russia
ambao wamepitishwa moja kwa moja kucheza Fainali hizo.
Kwenye Kundi
la Kanda ya Nchi za Marekani ya Kusini, Brazil
walifungwa Mechi yao ya kwanza kabisa na Chile lakini baada ya hapo hawakufungwa tena katika Mechi zao 13
wakishinda Mechi 10 na Sare 3 wakivuna Pointi 33 wakifuatiwa na Colombia wenye Pointi 24.
Zikiwa
zimebaki Mechi 4 kwa kila Timu, Timu nyingine ambazo zipo kwenye Nafasi za
kufuzu moja kwa moja kwenda Russia
ni Colombia, Uruguay na Chile.
Argentina, ambao wapo Nafasi ya 5, ikiwa
watabaki Nafasi hiyo hadi mwishoni itabidi wacheze Mechi ya Mchujo na Nchi
kutoka Kanda ya Oceania ili kufuzu kwenda Russia.
Jumatano Machi 29, 2017
Ecuador 2 –
0 Colombia
Chile 3 – 1 Venezuela
Brazil 3 – 0
Paraguay
Peru 2 – 1 Uruguay
MSIMAMO.
|
No comments:
Post a Comment