Timu ya
Arsenal imeondoshwa katika hatua ya 16 bora ya Mashindano ya Klabu Bingwa ulaya
msimu huu 2016/2017 wakiwa kwao Emirates Jijini London baada ya kucheza Mechi
ya Pili huku wakihitajika kupindua kipigo cha 5-1 cha Mechi ya Kwanza ili
kutinga hatua ya Robo Fainali na Wakajikuta wakitwangwa tena Bao 5-1 na Bayern
Munich ya Ujerumani.
|
Hivyo Bayern
Munich wanasonga Robo Fainali kwa Jumla ya Bao 10-2 kwa Mechi mbili.
Huu ni Msimu
wa 7 mfululizo kwa Arsenal kushindwa kuvuka Hatua hii ya makundi.
Arsenal
walianza Mechi hii kwa Dakika ya 19, Theo Walcott akawapa Arsenal Bao kwa Shuti
kali lililomshinda Kipa Neuer.
|
Dakika ya 52
Sentahafu wa Arsenal Koscielny alimwangusha Lewandowski na Refa kutoa Penati na
pia kumpa Kadi Nyekundu.
Penati hiyo
ilifungwa na Lewandowski na kisha Mvua
ya Magoli ya Bayern ikashuka kwa kupiga Bao nyingine 4 Dakika za 68, 78, 80 na
85 kupitia Arjen Robben, Douglas Costa na Arturo Vidal, Bao 2.
|
No comments:
Post a Comment