Kamanda wa
Polisi Mkoa wa Dodoma (Kushoto) akifafanua suala hilo.
Mfanyabiashara
na muagizaji wa pombe za viroba, Festo Mselia, amekutwa amejiua kwa kujipiga
risasi ikiwa ni siku moja baada ya Jeshi la Polisi kuendesha msako na kukamata
shehena ya pombe katika ghala alililokuwa akilimiki mjini Dodoma.
Katika vita
ya kupambana na matumizi ya pombe za vifungashio aina ya viroba vilivyopigwa
marufuku, jeshi la polisi mkoa wa Dodoma limefanikiwa kukamata shehena hiyo ya
katoni 1,400 ikiwa na thamani ya shilingi bilioni moja katika ghala la
mfanyabiashara huyo.
Mfanyabiashara
huyo aliyejiua ni wakala mkuu wa uagizaji na usambazaji wa pombe hizo akiwa
anamiliki 'store' ya Mselia Intapreses.
Awali katika
msako huo ulioongozwa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Dodoma, Lazaro Mambosasa,
alimtaka mfanyabiashara huyo kuendelea na shughuli zake, huku akiamuru shehena
hiyo isiuzwe wala kutumika wakati akisubiri maelekezo mengine.
Mambosasa
amesema jeshi linaendelea na uchunguzi kabla ua kutoa taarifa rasmi.
|
No comments:
Post a Comment