Baada ya
kukaa mahabusu kwa siku nne, Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA), Tundu Lissu
amesema kuwa maneno anayoshtakiwa kwa kuyatamka ni ya kweli na kuwa siyo kosa.
Lissu ambaye
yupo nje kwa dhamana ya Shilingi Milioni 20, amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi
Kisutu na kusomewa mashtaka manne ya kutoa maneno ya uchochezi na Wakili wa
Serikali Mwandamizi, Kishenyi Mutalemwa.
Awali, kabla
ya kupandishwa kizimbani mbunge huyo aligoma kula akiwa mahabusu ya polisi kwa
mujibu wa wakili wake, Peter Kibatala.
Kutoka kwa Lissu kulifuatia kasoro za
kuandaa kiapo kuwa mojawapo wa sababu zilizoifanya Mahakama hiyo kutupa
pingamizi la dhamana lililowekwa na upande wa Serikali.
Mbunge huyo
amepandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka manne ya kutoa kauli za uchochezi,
ambapo upande wa mashtaka uliwasilisha ombi la zuio la dhamana lililoambatana
na kiapo cha Mkuu wa Upelelezi wa Polisi Wilaya Ilala, Mrakabu Msaidizi (ASP),
Denis Mjumba.
Hata hivyo,
mahakama hiyo imetupa pingamizi la dhamana pamoja na mambo mengine kutokana na
kasoro katika kiapo hicho.
Akitoa
uamuzi wa pingamizi hilo, Hakimu Mkazi, Huruma Shaidi ameainisha mambo matatu
yaliyomfanya kulikataa pingamizi hilo na kuamua kumwachia kwa dhamana
mtuhumiwa.
Lissu
ametimiza masharti hayo na kudhaminiwa na Diwani wa Kata ya Tabata wa chama
hicho,CHADEMA, Patrick Asenga hivyo akaachiwa huru.
#Mwananchi.
|
No comments:
Post a Comment