Sakata la
dawa za kulevya bado lipo kwenye vichwa vya habari Tanzania ambapo Jumatatu ya
February 20,2017 imemuhusu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo
CHADEMA Freeman Mbowe aliyefika Polisi kwa mahojiano.
Jioni ya
Jumatatu Mbunge huyo wa Hai, Kilimanjaro alichukuliwa na Polisi kwenye msafara
wa magari yasiyopungua matatu ambapo iliripotiwa baadae kwamba Polisi
walikwenda kufanya upekuzi kwenye nyumba zake Kawe na Mikocheni kwa mujibu wa
Afisa habari wa CHADEMA.
Msemaji huyo
wa CHADEMA,Tumaini Makene alithibitisha Polisi kupekua nyumba zake na
kuandikisha maelezo ya majirani ambapo akasema kwenye mida ya saa sita usiku
huu Polisi wamemrudisha Mbowe kwenye kituo cha Polisi kati na wamemfungulia
jalada la Uchunguzi.
Siku ya
Jumamosi,February 18,2017, Kamanda wa Polisi kanda maalum ya Dar es Salaam, Simon Sirro alimpa
kiongozi huyo muda wa saa 48 za kujisalimisha vinginevyo watamtafuta kwa njia
wanazozijua wao.
Mbowe
aliitwa polisi kwaajili ya mahojiano kutokana na tuhuma za kujihusisha na
biashara ya madawa ya kulevya pamoja na kulisababishia usumbufu na gharama jeshi
la polisi.
|
No comments:
Post a Comment