Rais wa
Jamhuri ya Uganda Mhe. Yoweri Kaguta Museveni amemhakikishia Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli kuwa yupo tayari kuweka jiwe
la msingi la mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta kutoka Hoima nchini Uganda hadi
Bandari ya Tanga nchini Tanzania.
Mhe. Rais
Museveni amesema hayo jana tarehe 26 Februari, 2017 katika Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam wakati akiagana na mwenyeji
wake Mhe. Rais Magufuli baada ya kumaliza ziara yake rasmi ya kiserikali ya
siku 2 hapa nchini na kurejea Uganda.
“Tulikuwa
na mazungumzo mazuri na Mhe. Rais Magufuli, tumejadili mambo mengi hususani
kuhusu mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta, tumekubaliana na Mhe. Rais mambo
mengi, na sasa tutakwenda kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa mradi huo” alisema Mhe. Rais Museveni.
Mhe. Rais
Museveni aliwasili hapa nchini juzi asubuhi tarehe 25 Februari, 2017 ambapo
alifanya mazungumzo na mwenyeji wake Mhe. Rais Magufuli na jana alitembelea
viwanda viwili vinavyomilikiwa na kampuni ya mfanyabiashara wa Tanzania Bw.
Said Salim Bakhresa ambavyo ni kiwanda cha uzalishaji wa unga wa ngano
kilichopo Buguruni na kiwanda cha uzalishaji wa juisi kilichopo Vingunguti
Jijini Dar es Salaam.
Licha ya
kuwekeza nchini Uganda Mfanyabiashara huyo pia amekuwa akipeleka bidhaa zake
kwa wingi nchini Uganda.
Pamoja na
Mhe. Rais Magufuli viongozi wengine waliokuwepo wakati wa kumuaga Mhe. Rais
Museveni ni pamoja Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe.
Kassim Majaliwa Majaliwa na Viongozi wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama.
|
No comments:
Post a Comment