Pichani Bangi ndani ya Mahindi.
Kamati ya
ulinzi na usalama ya wilaya ya Ngara mkoani Kagera ikiongozwa na Mkuu wa wilaya
hiyo Luteni Kanali Michael Mtenjele na
iliwalazimu kuacha magari yao njiani na kutumia usafiri kwa pikipiki kuelekea
kwenye mashamba ya kilimo cha bangi huko Kata ya Keza, tarafa ya Rulenge ambapo
Jumla ya ekari 20 zimebainika na kukamatwa watu wanne wanaojihusisha na kilimo
cha bangi katika mapori pamoja na misitu yaliyoko kitongoji cha Mulole kata
hiyo ya Keza.
|
Mkuu wa wilaya Ngara, Luteni Kanali Michael Mtenjele pichani kushoto sambamba na Katibu tawala wa Wilaya hiyo Vedastus Tibaijuka wakiipigwa butwaa kwenye shamba lililolimwa na kustawi Bangi katika Kata ya Keza,tarafa ya Rulenge.
|
Mwenye chupa
ya maji na sweta la bluu ni Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Ngara Aidan Bahama ambapo alilazimika kutambaa akishuka na kupanda milima
kuingia ndani ya mashamba ya bangi.
Picha na
habari by Shaaban Ndyamukama
|
No comments:
Post a Comment