KUNA
magonjwa mengi ambayo watu hukumbana nayo lakini leo tutajadili magonjwa ya
zinaa ambayo huwapa zaidi vijana japokuwa kuna wazee hukumbana nayo.
Magonjwa
haya huathiri sehemu za siri na huweza kusababisha muathirika kutopata mtoto
Vijana wenye umri kati ya miaka 10 hadi 24 wako katika hatari zaidi ya
maambukizi ya magonjwa hayo kwa kuwa wanapo balehe, hupata hisia au hamu ya
kujamiiana.
Hali hii
husababishwa na vichocheo au homoni zilizomo mwilini zinazosababisha hisia za
kufanya mapenzi.
Kuna aina
mbalimbali za magonjwa ya zinaa ambayo yamegawanywa katika makundi kutokana na
dalili zake.
KUNDI LA
KWANZA
Kundi hili
ni magonjwa yenye dalili za kutokwa usaha au majimaji sehemu za siri (ukeni na
uumeni) ambayo ni kisonono, Trichomonas na Candida.
KUNDI LA
PILI
Ni la
magonjwa ya zinaa ambayo dalili zake ni kutokwa na vidonda, ambayo ni kaswende
na malengelenge sehemu za siri.
KUNDI LA TATU
Hili ni magonjwa yenye dalili za
kutokwa na uvimbe ambayo ni mitoki na pangusa sehemu za siri.
Mtu anaweza
kuwa na zaidi ya ugonjwa mmoja wa zinaa kwa wakati mmoja. Kujitokeza dalili za
ugonjwa wa zinaa hutegemea aina ya ugonjwa, jinsi na kinga ya mwili.
Hatari kubwa
ya makundi yote ya magonjwa hayo ni kwa wanawake kwani asilimia 60 mpaka
70 (ya wanawake) wenye kisonono
hawaoneshi dalili yoyote wakati wanaume ni kati ya asilimia 10 na 15.
Hivyo ni
muhimu kwa kijana wa kiume akiona dalili za ugonjwa kumueleza mwenzi wake wa
kike aliyejamiiananaye ili wote waende kwenye kituo cha huduma ya afya kwa uchunguzi
na tiba.
DALILI KWA
MWANAMKE
Mwanamke aliyekumbwa na maambukizi ya ugonjwa wa zinaa mara nyingi
hujisikia maumivu chini ya kitovu au kutokwa na usaha au majimaji yenye harufu
mbaya sehemu za siri.
Anaweza kuwashwa sehemu za siri au akatokwa na vidonda na
vipele kwenye nyeti zake, mdomoni na sehemu nyingine za mwili.
Wakati wa
kujamiiana anaweza kusikia maumivu au akawa amevimba mitoki, kuota mafindofindo
sehemu za siri na kukojoa mara kwa mara kunakoambatana na muwasho au maumivu.
DALILI ZA
UGONJWA WA ZINAA KWA WANAUME
Dalili za
tatizo hili kwa wanaume ni kujisikia maumivu wakati wa kukojoa au kutokwa na
usaha sehemu ya mbele kwenye dhakari.
Mgonjwa atasikia maumivu makali sehemu za
siri wakati wa kukojoa; atatokwa na usaha pamoja na kuwa na vidonda sehemu za siri na mdomoni na atavimba
mitoki na kupata malengelenge sehemu za
siri. Kwa ushauri wasiliana na mtaalamu
kwa namba za simu za hapo juu.
|
No comments:
Post a Comment