Shirikisho
la soka Ulimwenguni (FIFA) hapo jana February 09,2017 limetoa orodha mpya ya ubora wa viwango
vya soka Duniani kwa nchi Wanachama , na Vinara wake bado ni Argentina
wakifuatia Brazil na kwa Afrika ni Misri ndio wapo juu kabisa huku Tanzania
ikishuka Nafasi 2 na kukamata Namba 158.
5 Bora
kwenye orodha hiyo zimebaki zile zile bila mabadiliko na nazo ni Argentina (1),
Brazil (2), Germany (3), Chile (4) na Belgium (5).
Kwa Afrika,
Nchi ambayo iko juu kabisa ni Misri, waliotolewa Fainali ya AFCON 2017, ambao
sasa wapo Nafasi ya 23 baada kupanda Nafasi 12 wakifuata Senegal walio Nafasi
ya 31 na Mabingwa Wapya wa Afrika ambao ni Cameroon, wapo Nafasi ya 33 baada
kupaa Nafasi 29.
Listi
nyingine ya FIFA/Coca Cola Ubora Duniani itatolewa itatolewa Tarehe 9 Machi
2017.
Orodha hiyo
ni;
- Argentina
- Brazil
- Germany
- Chile
- Belgium
- France
- Colombia
- Portugal
- Uruguay
- Spain
- Switzerland
- Wales
- England
- Poland
- Italy
- Croatia
- Mexico
- Peru
- Costa Rica
- Iceland
Kwa upande
wa Afrika, Uganda bado wanaendelea kuongoza kwa Afrika Mashiriki wakiwa nafasi
ya 17 kwa Afrika na 75 duniani wakifuatiwa na Kenya waliopo nafasi ya 20 Afrika
na 87 duniani wakati Rwanda wako nafasi ya 27 Afrika na 100 duniani na Burundi
nafasi ya 40 Afrika na 138 duniani.
Kwa upande
wa Afrika, Misri wamekuwa vinara kwa kukwea kwa nafasi 12 na kutua kileleni
wakiwa nafasi ya 23, wakifuatiwa na Senegal walioko nafasi ya 31 huku mabingwa
wa michuano ya Mataifa ya Afrika Cameroon nao wakikwea kwa nafasi 29 mpaka
nafasi ya 33 duniani.
|
No comments:
Post a Comment