Mkurugenzi
Mtendaji wa Twaweza, Aidan Eyakuze, akizungumza na wanahabari (hawapo pichani).
UTAFITI wa taasisi ya Twaweza umeonyesha kuwa asilimia 88 ya wananchi
nchini wanataka majadiliano ya vikao vya Bunge yarushwe moja kwa moja bila
kujali gharama yoyote, wakati asilimia 12 tu wakisema wanadhani suala la kubana
matumizi ni sababu ya kutorusha vipindi vya bunge moja kwa moja.
Aidha,
utafiti huohuo umeonyesha kwamba asilimia 95 ya wananchi wanaunga mkono uhuru
wa maoni na kupata taarifa kwani wanasema ni haki yao kuikosoa serikali pale
ambapo wanaona imekosea.
Hayo
ameyasema leo Mkurugenzi Mtendaji wa Twaweza, Aidan Eyakuze, alipokuwa
akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam aliposema utafiti huo ni takwimu
za sauti za wananchi zinazoonyesha kuunga mkono wajibu wa vyombo vya habari
katika kuiwajibisha serikali.
Amesema
wananchi pia wanaunga mkono demokrasia kwani takwimu za hivi karibuni
zinaonyesha asilimia 69 ya walichagua demokrasia kuliko aina nyingine ya
serikali kwa takwimu za mwaka 2014.
Aidha
takwimu zinaonyesha asilimia 77 ya wananchi wa kawaida wanatakiwa wawe na uwezo
wa kupata taarifa zinazoshikiliwa na mamlaka za umma huku asilimia 23 wakisema
ni wale tu wanaofanya kazi kwenye mamlaka za umma ndiyo waruhusiwe kupata
taarifa hizo.
Na kwa
upande wa asilimia 80 wanasema upatikanaji wa taarifa hizo kwa wananchi
utasaidia kupunguza vitendo vya rushwa huku asilimia 20 wakisema watumishi wa
umma watatafuta njia nyingine za kuficha maovu yao.
Alifafanua
kuwa takwimu hizo ni za hivi karibuni za utafiti zilizokusanywa na Twaweza
baada ya kutiwa saini kwa sheria mpya ya huduma za vyombo vya habari.
Na Denis
Mtima/GPL
|
No comments:
Post a Comment