Akizungumza mbele ya Wanahabari
mapema leo (hawapo pichani) ndani ya Ukumbi wa
Idara ya Habari MAELEZO,Mwenyekiti wa Tanzania Bloggers Network (TBN),Joachim Mushi amesema kuwa mkutano huo
unatarajiwa kufanyika kuanzia Desemba 5
na 6 ,2016 hapa hapa jijini Dar,ambao utawashirikisha wanachama wapatao 150 kutoka Tanzania Bara na
Visiwani.Mushi alisema kuwa katika
mkutano huo Mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri wa Habari,Michezo,Utamaduni na Sanaa Mh Nape
Mosses Nnauye.
"Mgeni rasmi
anaetarajiwa kufungua mkutano huo ni Waziri Nape Nnauye,lengo kuu la mkutano huo likiwa ni kupeana elimu na
kubadilishana mawazo juu ya
uendeshaji wa Mitandao ya Kijamii kwa manufaa,upashaji habari kwa kutumia mitandao yao kwa kuzingatia maadili
na namna ya kunufaika na mitandao
hiyo kwa waendeshaji",alisema Mushi.
Alisema kuwa
uendeshaji wa Mitandao baadhi yao wanaifanya ni kama ajira nyingine,hivyo kimsingi lazima wakubali kuwa
mitandao hii imekuwa tegemeo kubwa la
kusambaza habari mbalimbali tena kwa muda mfupi tangu kutokea kwa tukio fulani,hivyo kuna kila
sababu ya kuendelea kuwapiga
msasa wanaoiendesha ili kupunguza matumizi mabaya ya mitandao hii.
Mkutano
huo utakaokuwa wa aina yake na kuiandika historia tangu kuanza kwa mitandano ya Kijamii hapa nchini,umedhaminiwa
na Benki ya NMB ambaye ni mdhamini mkuu
,NHIF, SBL, PSPF na Coca Cola.
|
No comments:
Post a Comment