Amiri Jeshi
Mkuu Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akichukua maelezo kutoka kwa maafisa na askari wa Jeshi la Magereza
alipofanya ziara ya kustukiza katika Gereza la Ukonga jijini Dar es salaam leo
Novemba 29, 2016.
|
Baadhi ya
maafisa na askari wa Jeshi la Magereza wakimsikiliza Rais Dkt John Pombe
Magufuli alipofanya ziara ya kustukiza katika Gereza la Ukonga jijini Dar es
salaam Jumanne, Novemba 29, 2016.
|
Askari
wakiwa na shauku ya kutoa kero zao mbele ya Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt John
Pombe Joseph Magufuli alipoongea na maafisa na askari wa Jeshi la Magereza
alipofanya ziara ya kustukiza katika Gereza la Ukonga jijini Dar es salaam leo
Novemba 29, 2016.
|
Mkuu wa
gereza la Ukonga akieleza changamoto za kazi Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt John
Pombe Joseph Magufuli alipofanya ziara
ya kustukiza katika Gereza la Ukonga jijini Dar es salaam Jumanne,Novemba 29,
2016.
|
Amiri Jeshi
Mkuu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli,
Jumanne tarehe 29 Novemba , 2016 amefanya ziara ya kushtukiza katika Gereza la
Ukonga jijini Dar Es Salaam na kupiga
marufuku uuzwaji wa sare za majeshi nchini na watu binafsi na kutaka wale wote
wanaouza sare hizo wazikabidhi kwa majeshi husika mara moja.
Rais
Magufuli amepiga marufuku hiyo kufuatia maelezo kutoka kwa baadhi ya askari wa
Jeshi la Magereza kuwa wamekuwa wakinunua sare za jeshi hilo kutoka kwa watu
binafsi kinyume na taratibu za majeshi nchini na kuvitaka vyombo vya ulinzi na
usalama kuwachukulia hatua mara moja wale wote watakaobainika kuuza sare za
majeshi ya hapa nchini
Hali
kadhalika Rais magufuli amepiga marufuku kwa majeshi yote nchini kuingia ubia
na watu binafsi kupangisha ama kuuza maeneo yao kwa ajili ya kufanya biashara
na kutaka maeneo yote ya majeshi yabaki katika jeshi husika.
''Haiwezekani
sare za majeshi yetu hapa nchini kuuzwa na watu binafsi hilo haliwezekani kamwe
labda baada ya kumaliza muda wangu , amesema Rais magufuli''
|
Aidha Rais Magufuli ametoa shilingi 10 bilioni kwa Jeshi la Magereza kwa ajili ya kujenga nyumba mpya zitakazotumika kwa ajili ya makazi ya askari wa Jeshi la Magereza katika Gereza la Ukonga jijini Dar es salaam.
Hatua hiyo inafuatia kilio cha askari Magereza kuwa wengi wao wamekuwa wakiishi uaraiani kitu ambacho ni tofauti na taratibu za majeshi nchini na hata kuzorotesha utendaji kazi wa askari wa Jeshi hilo.
Amiri Jeshi Mkuu na Rais Dkt. John Pombe Magufuli pia ameagiza Jeshi la Magereza kuhakikisha wafungwa wanatumika katika uzalishaji mali badala ya mfumo wa sasa ambapo baadhi ya wafungwa wamekuwa wakitutumia rasilimali za serikali bila kuzifanyia kazi.
Rais Magufuli amewahakikishia Maafisa na Askari wa Jeshi la Magereza kuwa serikali itaendelea kuboresha maslahi yao na vitendea kazi kama inavyofanya kwa majeshi mengine nchini.
|
Amiri Jeshi
Mkuu Rais Dkt John Pombe Joseph Magufuli akiongea na baadhi ya maafisa na
askari wa Jeshi la Magereza alipofanya ziara ya kustukiza katika Gereza la
Ukonga jijini Dar es salaam Jumanne Novemba 29, 2016.
PICHA NA
IKULU.
|
No comments:
Post a Comment