Kabla ya
kutangaza matokeo hayo, katibu Mtendaji wa NECTA, Dk. Charles Msonde
ameyazungumzia Matukio Sita ya udanganyifu yaliyotokea katika Mtihani wa Darasa
la saba 2016.
1. Moja ya
matukio ya udanganyifu ni pamoja na la
shule ya msingi Tumaini Sengerema ambapo mmiliki wa shule akishirikiana
na wasimamizi alifanya mtihani na kuwapa majibu watahiniwa, wakayaandika kwenye
sare zao wakaingia nayo kwenye chumba cha mtihani.
2. Shule ya
little flower ambayo iko Serengeti, mwalimu mkuu akishirikiana na wasimamizi
waliharibu mtihani wakaufanya na wakawapatia majibu wanafunzi, katika shule
hiyo afisa wa baraza alipokuwa akifanya ufuatiliaji wa mitihani alimkamata
mwalimu wa shule hiyo ambaye ni msimamizi akiwapa wanafunzi majibu.
3. Shule ya
mihamakumi ambayo iko Sikonge mkoani Tabora, walimu walichukua form za kujibia
mitihani, wanafunzi wanaingia chumba cha mtihani kutimiza wajibu tu baadae
walimu wanachukua zile karatasi na kuanza kutoa majibu wao wenyewe
4.Shule ya
Kashi Manyara, mwalimu alijificha chooni akiwa amepanga njama na mtahiniwa
mmoja kwamba atoke na karatasi ya maswali ambapo mwalimu atafanya na baadaye
mwanafunzi arudi chooni kuchukua majibu.
5. Shule ya
St. Getrude Ruvuma, mwalimu mkuu na walimu kadhaa walifanya njama kuwaonyesha
wanafunzi wote ambapo walipanga walimu wakae bwenini na kwenye nyumba ya
mwalimu na wakaweka kikundi cha wanafunzi kadhaa ambao watakuwa wanapeleka
maswali na baadae kuyaendea.
6. Shule
kondi pamoja na kasandalala Sikonge watahiniwa walikuwa wote wanakosa kwa namna
moja.
|
No comments:
Post a Comment