Profesa
Andrea Swai
___________________________________________________________
SODA, chumvi
na soda vinaongoza kwa kusababisha magonjwa yasiyo ya kuambukiza ikiwamo
shinikizo la damu, MTANZANIA limeelezwa.
Utafiti
uliofanywa na Chama cha Wagonjwa wa Kisukari Tanzania unaonyesha asilimia 27 ya
Watanzania wamebainika kuwa na shinikizo la damu.
Akizungumza
na Jukwaa la Waandishi wa Habari na Wahariri wa Kupambana na magonjwa
yasiyokuwa ya kuambukiza Tanzania (TJNCDF), Profesa Andrea Swai alisema
magonjwa yasiyoambukiza ndiyo yanayoongoza kwa idadi kubwa ya vifo.
Alisema
asilimia tisa ya Watanzania wote wamebainika kuwa na ugonjwa wa kisukari huku
ugonjwa wa saratani ukiongoza mara mbili ya wagonjwa wanaopokelewa hospitalini.
“Magonjwa
yasiyokuwa ya kuambukiza ndiyo yanaongoza kwa vifo na hii inatokna na vyakula
tunavyokula ikiwa ni pamoja na chumvi, soda na chips,” alisema Profesa Swai.
Alisema ili
kupunguza vifo vinavyotokana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza ni lazima
waandishi wa habari kutumia kalamu zao vema ili kuweza kuhabarisha umma.
Alisema kila
mmoja anajukumu la kupambana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza kwa kuzingatia
anafanya mazoezi ya kutosha ili kuimarisha afya ya mwili wake.
“Ifike
wakati tuwe na utamaduni wa kufanya mazoezi kwa ajili ya viungo vyetu hii
itatusaidia kupunguza magonjwa yasiyo ya kuambukiza,” alisema Profesa Swai.
|
No comments:
Post a Comment