Na George
Binagi-GB Pazzo
Mkuu wa mkoa
wa Mwanza, John Mongella, amewataka Watumiaji wa barabara mkoani Mwanza,
kuzingatia sheria za usalama barabarani jambo ambalo litasaidia juhudi za
kupambana na ajali kufanikiwa.
Mongella
ametoa kauli hiyo hii Jana,Oktoba 24,2016, kwenye uzinduzi wa maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa
Usalama Barabarani mkoani Mwanza, uliofanyika katika Uwanja wa Furahisha Jijini
Mwanza, ambapo elimu ya usalama barabarani itaendelea kutolewa kwenye
maadhimisho hayo kwa juma zima.
Amesema
watumiaji wote wa barabara wanao wajibu wa kufuata sheria za usalama barabarani
huku akikemea tabia ya baadhi ya abiria wanaowahimiza madereva kuendesha vyombo
vyao kwa mwendo kasi.
Akizungumza
kwa niaba ya watumiaji wa barabara, Makamu Mwenyekiti wa Waendesha bodaboda
mkoani Mwanza, Seifu Kagoma, amesema kila mtumiaji wa barabara anao wajibu wa
kuwa na tahahadhali awapo barabarani badala ya kusubiri wajibu huo kutoka kwa
mwenzake.
Maadhimisho
ya wiki ya usalama barabarani hufanyika kila mwaka nchini lengo likiwa ni kutoa
elimu ya matumizi sahihi na salama ya barabara kwa makundi yote ya watumiaji wa
barabara ambapo mwaka huu 2016 kitaifa yalifanyika mkoani Geita kuanzia Septemba 29
hadi Oktoba Mosi ambapo kauli mbiu yake ni “Hatutaki ajali, tunataka kuishi
salama”.
|
No comments:
Post a Comment