Ushindi wa
leo (October 23, 2016), ni ushindi wa nne mfululizo kwa Simba SC huku ukiwa ni
ushindi wao wa tisa katika mechi 11 walizocheza msimu huu 2016/2017 -hivyo
kufikisha pointi 29 na sasa wanawazidi Mabingwa watetezi, Yanga SC walioa
nafasi ya pili kwa tofauti ya pointi nane,wakiwa na Pointi 21.
|
Mchezo wa
leo, Magoli ya Simba SC yamefungwa na Muzamiru Yassin ambaye alinza kuifunga
goli la kwanza dakika ya 43 baada ya kupokea pasi nzuri kutoka kwa Fredick
Blagnon.
|
Laudit
Mavugo aliyeingia kutoka benchi kuchukua nafasi ya Blagnon aliifungia Simba SC bao
la pili dakika ya 52 akitumia vyema pasi ya Ibrahim Mohammed.
|
Bao la tatu
la Simba SC lilifungwa na Muzamiru Yassin dakika ya 74 na kuhitimisha ushindi
uliokuwa ukisubiriwa na mashabiki wa Simba SC baata ya timu yao kucheza mechi
nyingi bila ushindi mbele ya Toto Africans.
|
No comments:
Post a Comment